15 – Mke mkorofi

Jengine ni kwamba kuna mwanamke mkorofi. Mke mkorofi ni yule ambaye anafanya ukorofi katika maisha ya mumewe. Yeye haridhii urafiki na wala hatosheki na kidogo. Bali yeye ni mwenye kupindukia kwa kule kuomba kukamilishiwa mambo ya kifedha. Hana subira juu ya uchache wa hali ya pesa na hana subira juu ya hali ya kiafya. Matokeo yake atamtia dhiki mume wake mpaka amtimizie matamanio na matakwa yake. Anamuomba mume wake asichokiweza. Yeye anachojali ni nafsi na furaha yake tu na wala hamuhifadhi mume wala nyumba yake. Mara nyingi mwanamke kama huyu huishilia talaka.

  • Mhusika: Shaykh Jamaal bin Furahyaan al-Haarithiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Twalaaq – asbaabuhu wa ´ilaajuh, uk. 33-34
  • Imechapishwa: 15/04/2024