Abu Qataadah al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliulizwa kuhusu kufunga siku ya ´Arafah ambapo akajibu:
“Hufuta madhambi ya mwaka uliopita na mwaka ujao.”[1]
Ameipokea Muslim.
Hadiyth hii ni dalili ya fadhilah ya kufunga siku ya ´Arafah na thawabu kubwa mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala), kwa sababu kufunga siku hiyo kunafuta madhambi ya miaka miwili. Kufunga siku ya ´Arafah kunapendekezwa kwa wakazi walioko majumbani. Kuhusu mahujaji haipendekezwi kufunga siku hiyo. Badala yake napendekezwa afungue akifuata mfano wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa hivyo inampasa muislamu ambaye ni mkazi afanye pupa ya kufunga siku hii tukufu ili kupata thawabu.
[1] Muslim (1162).
- Muhusika: Shaykh ´Abdullaah bin Swaalih al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahaadiyth ´Ashrah Dhil-Hijjah wa Ayaam-it-Tashriyq, uk. 33
- Imechapishwa: 13/05/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket