Abu Qataadah al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliulizwa kuhusu kufunga siku ya ´Arafah ambapo akajibu:
“Hufuta madhambi ya mwaka uliopita na mwaka ujao.”[1]
Ameipokea Muslim.
Hadiyth hii ni dalili ya fadhilah ya kufunga siku ya ´Arafah na thawabu kubwa mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala), kwa sababu kufunga siku hiyo kunafuta madhambi ya miaka miwili. Kufunga siku ya ´Arafah kunapendekezwa kwa wakazi walioko majumbani. Kuhusu mahujaji haipendekezwi kufunga siku hiyo. Badala yake napendekezwa afungue akifuata mfano wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa hivyo inampasa muislamu ambaye ni mkazi afanye pupa ya kufunga siku hii tukufu ili kupata thawabu.
[1] Muslim (1162).
- Muhusika: Shaykh ´Abdullaah bin Swaalih al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahaadiyth ´Ashrah Dhil-Hijjah wa Ayaam-it-Tashriyq, uk. 33
- Imechapishwa: 13/05/2025
Abu Qataadah al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliulizwa kuhusu kufunga siku ya ´Arafah ambapo akajibu:
“Hufuta madhambi ya mwaka uliopita na mwaka ujao.”[1]
Ameipokea Muslim.
Hadiyth hii ni dalili ya fadhilah ya kufunga siku ya ´Arafah na thawabu kubwa mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala), kwa sababu kufunga siku hiyo kunafuta madhambi ya miaka miwili. Kufunga siku ya ´Arafah kunapendekezwa kwa wakazi walioko majumbani. Kuhusu mahujaji haipendekezwi kufunga siku hiyo. Badala yake napendekezwa afungue akifuata mfano wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa hivyo inampasa muislamu ambaye ni mkazi afanye pupa ya kufunga siku hii tukufu ili kupata thawabu.
[1] Muslim (1162).
Muhusika: Shaykh ´Abdullaah bin Swaalih al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahaadiyth ´Ashrah Dhil-Hijjah wa Ayaam-it-Tashriyq, uk. 33
Imechapishwa: 13/05/2025
https://firqatunnajia.com/19-hadiyth-hufuta-madhambi-ya-mwaka-uliopita-na-mwaka-ujao/