Wanazuoni wanaona kuwa mtu asikate kumfundisha yeyote kwa sababu ya kuwa hana nia sahihi. Sufyaan na wengineo wamesema:

”Kule kutafuta kwao elimu ni nia.”

Wamesema tena:

”Tulitafuta elimu kwa ajili ya asiye Allaah, lakini ikakataa isipokuwa iwe kwa ajili ya Allaah.”

Maana yake ni kwamba mwisho wake ukawa ni kwa ajili ya Allaah (Ta´ala).

  • Muhusika: Imaam Yahyaa bin Sharaf an-Nawawiy (afk. 677)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tibyaan fiy Aadaabi Hamalat-il-Qur-aan, uk. 32
  • Imechapishwa: 26/08/2026