Swali 176: Je, inafaa kwa mwanamke anayemkalia eda mume wake kuwaosha watoto wake na kuwatia manukato? Je, inafaa kuposwa ilihali yuko ndani ya eda[1]?
Jibu: Haifai kwa mwanamke ambaye yuko katika eda ya kufiwa na mume wake kujitia manukato. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza jambo hilo. Lakini hapana vibaya kuwasogelea watoto wake na wageni wake pasi na kuchanganyikana nao katika hayo. Haijuzu kuposwa uposaji wa wazi mpaka pale atakapotoka katika eda. Hapana neno kumwashiria pasi na kumuwekea wazi. Amesema (Ta´ala):
وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ فِيمَا عَرَّضْتُم بِهِ مِنْ خِطْبَةِ النِّسَاءِ
“Wala si dhambi juu yenu katika ambayo mmedokezea ya kuposa wanawake hao.”[2]
Ameruhusu (Subhaanah) kumwashiria na hakuruhusu kumuwekea wazi. Yeye (Subhaanah) ana hekima kuu juu ya jambo hilo.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (22/203-204).
[2] 02:235
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 132
- Imechapishwa: 07/02/2022
Swali 176: Je, inafaa kwa mwanamke anayemkalia eda mume wake kuwaosha watoto wake na kuwatia manukato? Je, inafaa kuposwa ilihali yuko ndani ya eda[1]?
Jibu: Haifai kwa mwanamke ambaye yuko katika eda ya kufiwa na mume wake kujitia manukato. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza jambo hilo. Lakini hapana vibaya kuwasogelea watoto wake na wageni wake pasi na kuchanganyikana nao katika hayo. Haijuzu kuposwa uposaji wa wazi mpaka pale atakapotoka katika eda. Hapana neno kumwashiria pasi na kumuwekea wazi. Amesema (Ta´ala):
وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ فِيمَا عَرَّضْتُم بِهِ مِنْ خِطْبَةِ النِّسَاءِ
“Wala si dhambi juu yenu katika ambayo mmedokezea ya kuposa wanawake hao.”[2]
Ameruhusu (Subhaanah) kumwashiria na hakuruhusu kumuwekea wazi. Yeye (Subhaanah) ana hekima kuu juu ya jambo hilo.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (22/203-204).
[2] 02:235
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 132
Imechapishwa: 07/02/2022
https://firqatunnajia.com/176-makatazo-ya-kumposa-mwanamke-aliye-katika-eda/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)