83- Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) siku moja alipita karibu na soko la Madiynah akasimama na kusema: “Enyi watu wa sokoni! Kipi kimekufanyeni kushindwa!” Wakasema: “Vipi, ee Abu Hurayrah?” Akasema: “Mirathi ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) inagawanywa na nyinyi mko hapa. Kwa nini msende na nyinyi mjitwalie fungu lenu?” Wakasema: “Iko wapi?” Akasema: “Msikitini.” Wakatoka matiti. Abu Hurayrah akasimama palepale mpaka waliporudi.” Abu Hurayrah akawaambia: “Mna nini?” Wakasema: “Ee Abu Hurayrah! Tumefika msikitini na tukaingia ndani yake na hatujaona kitu kinachogawanywa.” Abu Hurayrah akawaambia: “Hamkumuona msikitini yeyote?” Wakasema: “Ndio. Tumewaona watu wanaswali, wengine wanasoma Qur-aan, wengine wanadarisishana ya halali na ya haramu.” Ndipo Abu Hurayrah akawaambia: “Ole wenu! Hiyo ndio mirathi ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)!”[1]
Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Awsatw” kwa cheni ya wapokezi nzuri.
[1] Nzuri kutoka kwa Swahabah.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/143)
- Imechapishwa: 29/04/2020
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)