Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:

Tunachokusudia hapa ni kuzindua juu ya misingi mibovu ya ´Aqiydah ambayo imepelekea kupotoka kutokana na elimu na kuamini yale aliyokuja nayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

MAELEZO

Kusudio la Shaykh-ul-Islaam (Rahimahu Allaah) kwa yale aliyoyataja katika fatwa hii ni kubainisha I´tiqaad ya watu wanaopindisha maana na wale wanaofata ujinga, kuonyesha kuwa ni I´tiqaad potofu na ya batili. Hili ndilo kusudio lake. I´tiqaad na misingi waliyojiwekea wenyewe na kuwaamrisha watu warejee kwayo ndiyo iliyoharibu akili, ikaharibu imani na kuzuia elimu, kwa sababu elimu ni kujua yale yaliyomo ndani ya Qur-aan na Sunnah. Ndiyo maana Ibn-ul-Qayyim (Rahimahu Allaah) amesema:

Basi izingatie na uitafakari Qur-aan ikiwa unataka uongofu

kwa kuwa elimu ipo chini ya kuizingatia na kuitafakari Qur-aan[1]

Amesema pia (Rahimahu Allaah):

Elimu ni Allaah amesema, Mtume Wake amesema na Maswahabah wamesema –

hao ndio wenye maarifa[2]

[1] an-Nuuniyyah (1/315).

[2] an-Nuuniyyah (2/279).

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaa al-Hamawiyyah, uk. 271
  • Imechapishwa: 28/07/2026