15. Wazushi siku ya Qiyaamah watabeba madhambi ya wafuasi wao

Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:

Allaah (´Azza wa Jall) amesema:

فَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّنِ افْتَرَىٰ عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا لِّيُضِلَّ النَّاسَ بِغَيْرِ عِلْمٍ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ

 “Ni nani dhalimu zaidi kuliko yute anayemtungia Allaah uongo ili apoteze watu pasi na elimu? Hakika Allaah hawaongozi watu madhalimu.” (06:144)

لِيَحْمِلُوا أَوْزَارَهُمْ كَامِلَةً يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۙ وَمِنْ أَوْزَارِ الَّذِينَ يُضِلُّونَهُم بِغَيْرِ عِلْمٍ ۗ أَلَا سَاءَ مَا يَزِرُونَ

 “Ili wabebe mizigo [ya madhambi] yao kamili Siku ya Qiyaamah na mizigo ya wale waliowapoteza bila ya elimu – Zindukeni! Uovu ulioje wanayoyabeba!” (16:25)

MAELEZO

Ili wabebe mizigo… – Bi maana wana madhambi sawa na wale waliowafuata katika Bid´ah zao. Tunamuomba Allaah usalama.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Fadhwl-il-Islaam, uk. 26
  • Imechapishwa: 02/11/2020