Maalik alikuwa akikosoa maneno mengi na kufutu na akisema juu ya yule mwenye kuingia katika mambo hayo:
“Ambaye anaropoka ni kama ngamia mwitu.”
Alikuwa akichukia kujibu maswali mengi na akisema:
“Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الرُّوحِ ۖ قُلِ الرُّوحُ مِنْ أَمْرِ رَبِّي وَمَا أُوتِيتُم مِّنَ الْعِلْمِ إِلَّا قَلِيلًا
“Wanakuuliza kuhusu roho. Sema: “Roho ni katika amri ya Mola wangu.” na hamkupewa ujuzi isipokuwa kidogo tu.”[1]
Hakutoa (Ta´ala) juu ya jambo hilo jibu lolote.”
Wakati mmoja aliulizwa juu ya mtu ambaye ni mtambuzi wa Sunnah kujadiliwe juu yake, akasema:
“Hapana. Asimulie Sunnah. Akikubaliwa ni vyema vinginevyo anyamaze.”
Amesema tena:
“Elimu ya mivutano na mijadala inazima nuru ya elimu.”
Amesema vilevile:
“Elimu ya mivutano inaufanya moyo kuwa msusuwavu na inapelekea chuki.”
Alikuwa akijibu juu ya maswali yanayouliziwa sana:
“Sijui.”
Imaam Ahmad alikuwa akifanya vivo hivyo. Licha ya haya Salaf na maimamu, kama vile Maalik, ash-Shaafi´iy, Ahmad na Ishaaq, wamebainisha namna ambavo Fiqh na hukumu zinatakiwa kuchukuliwa na kufahamika kwa njia fupi na ya mukhtasari.
[1] 17:85
- Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn bin Rajab al-Hanbaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bayaan Fadhwl ´Ilm-is-Salaf ´alaa ´Ilm-il-Khalaf, uk. 59-60
- Imechapishwa: 21/09/2021
Maalik alikuwa akikosoa maneno mengi na kufutu na akisema juu ya yule mwenye kuingia katika mambo hayo:
“Ambaye anaropoka ni kama ngamia mwitu.”
Alikuwa akichukia kujibu maswali mengi na akisema:
“Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الرُّوحِ ۖ قُلِ الرُّوحُ مِنْ أَمْرِ رَبِّي وَمَا أُوتِيتُم مِّنَ الْعِلْمِ إِلَّا قَلِيلًا
“Wanakuuliza kuhusu roho. Sema: “Roho ni katika amri ya Mola wangu.” na hamkupewa ujuzi isipokuwa kidogo tu.”[1]
Hakutoa (Ta´ala) juu ya jambo hilo jibu lolote.”
Wakati mmoja aliulizwa juu ya mtu ambaye ni mtambuzi wa Sunnah kujadiliwe juu yake, akasema:
“Hapana. Asimulie Sunnah. Akikubaliwa ni vyema vinginevyo anyamaze.”
Amesema tena:
“Elimu ya mivutano na mijadala inazima nuru ya elimu.”
Amesema vilevile:
“Elimu ya mivutano inaufanya moyo kuwa msusuwavu na inapelekea chuki.”
Alikuwa akijibu juu ya maswali yanayouliziwa sana:
“Sijui.”
Imaam Ahmad alikuwa akifanya vivo hivyo. Licha ya haya Salaf na maimamu, kama vile Maalik, ash-Shaafi´iy, Ahmad na Ishaaq, wamebainisha namna ambavo Fiqh na hukumu zinatakiwa kuchukuliwa na kufahamika kwa njia fupi na ya mukhtasari.
[1] 17:85
Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn bin Rajab al-Hanbaliy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Bayaan Fadhwl ´Ilm-is-Salaf ´alaa ´Ilm-il-Khalaf, uk. 59-60
Imechapishwa: 21/09/2021
https://firqatunnajia.com/15-salaf-na-fatwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)