Ni kuamini kwa kukata na kusadikisha mipango na makadirio ya Allaah. Hilo limekusanya:
1 – Kuamini kuwa Allaah aliyajua mambo kabla ya kuumbwa kwake na aliyajua yatayokuwa huko mbele. Yeye (Subhaanah) anayajua yaliyokuweko, yatayokuweko na yasiyokuweko iwapo yangelikuweko basi yangelikuwa namna gani. Amesema (Ta´ala):
إِنَّ اللَّـهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
“Hakika Allaah kwa kila kitu ni Mjuzi.”[1]
وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
“Naye juu ya kila jambo ni Mjuzi.”[2]
أَلَمْ تَعْلَمْ أَنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ
“Je, hujui kwamba Allaah anajua yale yote yaliyomo katika mbingu na ardhi?”[3]
عَالِمِ الْغَيْبِ ۖ لَا يَعْزُبُ عَنْهُ مِثْقَالُ ذَرَّةٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ
“Mjuzi wa mambo yaliyofichikana; hakuna kinachofichikana Kwake ingawa chenye uzito wa chembe mbinguni wala ardhini.”[4]
[1] 08:75
[2] 02:29
[3] 22:70
[4] 34:03
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Iymaan – Haqiyqatuhu wa Nawaaqidhwuh, uk. 24
- Imechapishwa: 26/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)