Abu Ma´mar al-Qutwiy´iy amesema:
”Mwisho wa maneno ya Jahmiyyah ni kwamba hakuna juu ya mbingu mungu yeyote.”
Ameipokea Abu Haatim.
Bishr al-Haafiy amesema:
”Tunaamini kwamba Allaah amelingana juu ya ´Arshi Yake, kama Anavyotaka, na kwamba Yeye ni Mjuzi wa kila mahali.”
Ameipokea Ibn Battwah na wengineo.
Harb bin Ismaa´iyl amesema:
”Nilimuuliza Ishaaq bin Raahawayh: ”Unasemaje juu ya maneno Yake Allaah (Ta´ala):
مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَىٰ ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ
“Hauwi mnong’ono wa watatu isipokuwa Yeye ni wa nne wao.”[1]
Akajibu: ”Popote ulipo basi Yeye yukaribu zaidi nawe kuliko mshipa wa shingo na wakati huohuo Yeye ametengana mbali na viumbe Vyake.” Amemnukuu Ibn-ul-Mubaarak, ambaye amesema kuwa Yuko juu ya ´Arshi Yake na ametengana mbali na viumbe Wake, kisha akasema: ”Kilicho juu zaidi ya hayo na kilicho na nguvu zaidi ni maneno Yake (Ta´ala):
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[2]
Ameipokea al-Khalaal katika “as-Sunnah”.
Yuusuf bin Muusa, na si al-Qattwaan, ameeleza:
”Ilisemwa kuambiwa ´Abdillaah Ahmad bin Hanbal: “Allaah yuko juu ya mbingu ya saba juu ya ´Arshi Yake, mbali na viumbe Vyake, ilihali uwezo Wake na ujuzi Wake viko kila mahali?” Akajibu: ”Ndiyo.”
Ameipokea al-Khallaal katika ”as-Sunnah”.
Dhuun-Nuun al-Miswriy amesema:
”Nuru Yake imezing’arisha mbingu, uso Wake umeangaza giza, utukufu Wake umefichwa na macho na humnong´oneza juu ya ´Arshi Yake ndimi za vifuani.”
Ameipokea Abush-Shaykh katika ”al-´Adhwamah”.
Ahmad bin Salamah amesimulia ya kwamba amemsikia Ishaaq bin Raahuuyah akisema:
”Nilikutanishwa na huyu mzushi – akimaanisha Ibraahiym bin Abiy Swaalih – kwenye kikao cha gavana ´Abdullaah bin Twaahir. Gavana akaniuliza kuhusiana na Hadiyth za Kushuka anbapo nikazisoma. Akasema Ibn Abiy Saalih: “Nimememkufuru Mola anayeshuka kutoka mbingu moja hadi mbingu nyingine.” Ndipo nikasema: “Nimemwamini Mola anayefanya atakacho.”
Ameipokea al-Bayhaqiy na wengineo.
[1] 58:7
[2] 20:5
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad bin ´Abdil-Haadiy al-Maqdisiy (afk. 744)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Kalaam ´alaa Mas-alat-il-Istiwaa’ ´alaal-´Arsh, uk. 63-65
- Imechapishwa: 23/12/2025
Abu Ma´mar al-Qutwiy´iy amesema:
”Mwisho wa maneno ya Jahmiyyah ni kwamba hakuna juu ya mbingu mungu yeyote.”
Ameipokea Abu Haatim.
Bishr al-Haafiy amesema:
”Tunaamini kwamba Allaah amelingana juu ya ´Arshi Yake, kama Anavyotaka, na kwamba Yeye ni Mjuzi wa kila mahali.”
Ameipokea Ibn Battwah na wengineo.
Harb bin Ismaa´iyl amesema:
”Nilimuuliza Ishaaq bin Raahawayh: ”Unasemaje juu ya maneno Yake Allaah (Ta´ala):
مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَىٰ ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ
“Hauwi mnong’ono wa watatu isipokuwa Yeye ni wa nne wao.”[1]
Akajibu: ”Popote ulipo basi Yeye yukaribu zaidi nawe kuliko mshipa wa shingo na wakati huohuo Yeye ametengana mbali na viumbe Vyake.” Amemnukuu Ibn-ul-Mubaarak, ambaye amesema kuwa Yuko juu ya ´Arshi Yake na ametengana mbali na viumbe Wake, kisha akasema: ”Kilicho juu zaidi ya hayo na kilicho na nguvu zaidi ni maneno Yake (Ta´ala):
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[2]
Ameipokea al-Khalaal katika “as-Sunnah”.
Yuusuf bin Muusa, na si al-Qattwaan, ameeleza:
”Ilisemwa kuambiwa ´Abdillaah Ahmad bin Hanbal: “Allaah yuko juu ya mbingu ya saba juu ya ´Arshi Yake, mbali na viumbe Vyake, ilihali uwezo Wake na ujuzi Wake viko kila mahali?” Akajibu: ”Ndiyo.”
Ameipokea al-Khallaal katika ”as-Sunnah”.
Dhuun-Nuun al-Miswriy amesema:
”Nuru Yake imezing’arisha mbingu, uso Wake umeangaza giza, utukufu Wake umefichwa na macho na humnong´oneza juu ya ´Arshi Yake ndimi za vifuani.”
Ameipokea Abush-Shaykh katika ”al-´Adhwamah”.
Ahmad bin Salamah amesimulia ya kwamba amemsikia Ishaaq bin Raahuuyah akisema:
”Nilikutanishwa na huyu mzushi – akimaanisha Ibraahiym bin Abiy Swaalih – kwenye kikao cha gavana ´Abdullaah bin Twaahir. Gavana akaniuliza kuhusiana na Hadiyth za Kushuka anbapo nikazisoma. Akasema Ibn Abiy Saalih: “Nimememkufuru Mola anayeshuka kutoka mbingu moja hadi mbingu nyingine.” Ndipo nikasema: “Nimemwamini Mola anayefanya atakacho.”
Ameipokea al-Bayhaqiy na wengineo.
[1] 58:7
[2] 20:5
Muhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad bin ´Abdil-Haadiy al-Maqdisiy (afk. 744)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Kalaam ´alaa Mas-alat-il-Istiwaa’ ´alaal-´Arsh, uk. 63-65
Imechapishwa: 23/12/2025
https://firqatunnajia.com/15-kikao-kwa-gavana/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket