991- Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga siku moja katika njia ya Allaah, basi Allaah ataweka kati yake yeye na Moto kama mfano wa masafa kati ya mbingu na ardhi.”[1]
Ameipokea at-Tirmidhiy kupitia kwa al-Waliyd bin Jamiyl, kutoka kwa Qaasim bin ´Abdir-Rahmaan, kutoka kwa Abu Umaamah. at-Tirmidhiy amesema:
“Hadiyth geni.”
Wanachuoni wengi wanaonelea kuwa Hadiyth hizi zinahusiana na fadhilah za kufunga katika Jihaad, jambo ambalo at-Tirmidhiy na wengineo wameliwekea mlango. Wanachuoni wengine wameonelea kuwa kila swawm inayofungwa kwa ajili ya Allaah ni katika njia ya Allaah.
[1] Nzuri kupitia zengine.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (01/581)
- Imechapishwa: 06/06/2018
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)