129. Kufaa kunyanyua mikono wakati wa kumuombea du´aa maiti makaburini

120 – Inajuzu kuinua mikono wakati kumuombea du´aa maiti. Hilo ni kutokana na Hadiyth ya ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) aliposema:

”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) usiku mmoja alitoka, nikamtuma Bariyrah nyuma yake aone alikoenda. Akasema: ”Alielekea upande wa Baqiy´ al-Gharqad, akasimama sehemu ya chini ya Baqiy´ kisha akainua mikono yake, kisha akaondoka. Bariyrah akarudi kwangu na kunijulisha. Asubuhi ilipopambazuka nikamuuliza: ”Ee Mtume wa Allaah, umetoka wapi usiku wa jana?” Akasema: ”Nilitumwa kwa watu wa Baqiy´ ili niwaombee du´aa.”

Ameipokea Ahmad (6/92), na imo katika ”al-Muwattwa´” (1/239-240), na kutoka humo an-Nasaa´iy (1/287) amepokea mfano wake, isipokuwa hakujatajwa ndani yake kuinua mikono. Cheni yake ya wapokezi ni nzuri.

Kuinua mikono kumethibiti katika kisa kingine cha ‘Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) kilichotangulia katika masuala ya 119.

  • Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz wa Bid´ahaa, uk. 246
  • Imechapishwa: 09/08/2026