Haya ndio makundi yaliyotajwa na mtunzi wa kitabu kisha akasema:
“Na mfano wao kama vile Ash´ariyyah ambao ni wafuasi wa al-Hasan bin Ismaa´iyl ash-Ash´ariy. Alikuwa mwanzoni mwa jambo lake akilimi katika madhehebu ya Mu´tazilah mpaka alipofikisha umri wa miaka arobaini kisha akatangaza kutubu kwake kutokamana na jambo hilo na akabainisha upotofu wa madhehebu ya Mu´tazilah na akashikamana na madhehebu ya Ahl-us-Sunnah – Allaah amrehemu. Kuhusu wale wanaojinasibisha naye walibakia katika madhehebu maalum yanayotambulika kama madhehebu ya Ashaa´irah. Hakuna wanachothibitisha katika sifa za Allaah isipokuwa saba peke yake hali ya kudai kuwa akili ndio imezifahamisha. Zilizosalia zote wanazipindisha maana. Zimetajwa katika shairi hili:
1 – Uhai.
2 – Mjuzi.
3 – Muweza.
4 – Mwenye kuzungumza.
5 – Matakwa.
6 – Usikizi.
7 – Uoni.
Wana Bid´ah nyinginezo kuhusu maana ya maneno, uwezo na mengineyo.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 163
- Imechapishwa: 22/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)