Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
93 – Hata hivyo haihitajii ´Arshi na vyenginevyo.
MAELEZO
Usifikiri maneno Yake (Ta´ala):
ثُمَّ اسْتَوَى عَلَى الْعَرْشِ ٌ
”… kisha Akalingana juu ya ´Arshi.”[1]
kuwa ni mwenye kuhitajia ´Arshi hiyo kama ambavyo kiumbe analingana juu ya kiumbe kingine. Allaah (´Azza wa Jall) amelingana juu ya ´Arshi na wakati huohuo si mwenye kuihitajia wala kitu kingine. Lakini viumbe wote ni wenye kumuhitajia Yeye:
إِنَّ اللَّـهَ يُمْسِكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ أَن تَزُولَا ۚ وَلَئِن زَالَتَا إِنْ أَمْسَكَهُمَا مِنْ أَحَدٍ مِّن بَعْدِهِ
“Hakika Allaah anazuia mbingu na ardhi zisiondoke na zikiondoka basi hakuna yeyote wa kuzishikilia baada Yake.”[2]
Yeye ndiye ambaye anazuia´Arshi, mbingu, ardhi na viumbe vyengine vyote kwa uwezo na nguvu Zake. Wao ndio wenye kumuhitajia, lakini Yeye (Subhaanahu wa Ta´ala) hawahitajii. Kwa sababu kitu kiko juu ya kingine, haina maana kwamba kile kilicho juu kinahitaji kilichoko chini yake. Mbingu ziko juu ya ardhi lakini hazihitaji ardhi.
[1]57:4
[2]35:41
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 125-126
- Imechapishwa: 10/11/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)