113 – Inapendekezwa kupapasa kichwa cha yatima na kumkirimu. Hilo ni kutokana na Hadiyth ya ´Abdullaah bin Ja´far aliyesema:

“Kama ungekuwa umeniona mimi, Qutham na ´Ubaydullaah bin ´Abbaas tulipokuwa watoto tukicheza. Tahamaki Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipita akiwa juu ya mnyama wake ambapo akasema: ”Muinueni huyu kwangu!”, akaniweka mbele yake. Akasema: ”Muinueni huyu kwangu!”, akaniweka nyuma yake. ´Ubaydullaah alikuwa mpendwa zaidi kwa ´Abbaas kuliko Qutham, lakini hakupata haya mbele ya ami yake kwa kumchukua Qutham na kumuacha yeye. Kisha alipapasa kichwa changu mara tatu. Kila alipompapasa alisema:

اللهم اخلف جعفرا في ولده

”Ee Allaah, mpe mrithi Ja´far katika watoto wake.”

Nikamuuliza ´Abdullaah: ”Qutham alipata nini?” Akasema: ”Alifariki hali ya kuwa shahidi.” Nikasema: ”Allaah na Mtume Wake wanajua zaidi kuhusu kheri.” Akasema: ”Ndio.”

Ameipokea Ahmad (1760) ambaye tamko ni lake, al-Haakim (1/372), al-Bayhaqiy (4/60) na cheni yake ya wapokezi ni nzuri. al-Haakim amesema: “Swahiyh.”

adh-Dhahabiy ameafikiana naye.

  • Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz wa Bid´ahaa, uk. 212
  • Imechapishwa: 30/07/2026