6 – Kukatika kwa yale yanayowajibisha wudhuu´
Sharti ya sita miongoni mwa sharti za kusihi kwa wudhuu´ ni kukatika kwa yale yanayowajibisha wudhuu´. Kwa mfano miongoni mwa mambo yanayowajibisha kutawadha ni kutokwa na mkojo. Wudhuu´ hausihi mpaka ukatike mkojo. Kwa mfano mtu akitawadha na huku mkojo unamtoka wudhuu´ wake hausihi. Kwa sababu hakijakatika kile kinachowajibisha. Bali ni lazima kwake kusubiri hadi kikatike kile kinachotoka nje kisha baada ya hapo ndio atawadhe. Mfano mwingine ikiwa mtu atatawadha na huku anatokwa na upepo, wudhuu´ wake hausihi. Bali anatakiwa kusubiri mpaka umalizike ule upepo unaotoka kisha baada ya hapo ndio atawadhe. Mfano wa tatu ikiwa anakula nyama ya ngamia. Katika hali hiyo anapaswa asubiri na asitawadhe mpaka atakapomaliza. Halafu baada ya hapo ndio atawadhe.
7 – Kujisafisha kwa maji au kwa kutumia mawe kabla yake
Sharti ya sita miongoni mwa sharti za kusihi kwa wudhuu´ ni kujisafisha kwa maji au kwa kutumia mawe kabla yake. Ni lazima mtu atangulize kujisafisha kwa maji au kwa mawe kabla ya kutawadha. Ima mtu ajisafishe maeneo hayo kwa kutumia maji au kwa kutumia mawe. Pindi atapotokwa na mkojo au kinyesi, basi ni lazima asafishe maeneo hayo kwa maji kabla ya kuanza kutawadha kwa njia ya kwamba aoshe ncha ya uume kwa maji na si kwamba aoshe uume wote. Anachotakiwa ni kusafisha yale pale nchani. Vivyo hivyo anatakiwa kuosha tupu ya nyuma kwa maji au kwa mawe.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 22
- Imechapishwa: 09/12/2021
6 – Kukatika kwa yale yanayowajibisha wudhuu´
Sharti ya sita miongoni mwa sharti za kusihi kwa wudhuu´ ni kukatika kwa yale yanayowajibisha wudhuu´. Kwa mfano miongoni mwa mambo yanayowajibisha kutawadha ni kutokwa na mkojo. Wudhuu´ hausihi mpaka ukatike mkojo. Kwa mfano mtu akitawadha na huku mkojo unamtoka wudhuu´ wake hausihi. Kwa sababu hakijakatika kile kinachowajibisha. Bali ni lazima kwake kusubiri hadi kikatike kile kinachotoka nje kisha baada ya hapo ndio atawadhe. Mfano mwingine ikiwa mtu atatawadha na huku anatokwa na upepo, wudhuu´ wake hausihi. Bali anatakiwa kusubiri mpaka umalizike ule upepo unaotoka kisha baada ya hapo ndio atawadhe. Mfano wa tatu ikiwa anakula nyama ya ngamia. Katika hali hiyo anapaswa asubiri na asitawadhe mpaka atakapomaliza. Halafu baada ya hapo ndio atawadhe.
7 – Kujisafisha kwa maji au kwa kutumia mawe kabla yake
Sharti ya sita miongoni mwa sharti za kusihi kwa wudhuu´ ni kujisafisha kwa maji au kwa kutumia mawe kabla yake. Ni lazima mtu atangulize kujisafisha kwa maji au kwa mawe kabla ya kutawadha. Ima mtu ajisafishe maeneo hayo kwa kutumia maji au kwa kutumia mawe. Pindi atapotokwa na mkojo au kinyesi, basi ni lazima asafishe maeneo hayo kwa maji kabla ya kuanza kutawadha kwa njia ya kwamba aoshe ncha ya uume kwa maji na si kwamba aoshe uume wote. Anachotakiwa ni kusafisha yale pale nchani. Vivyo hivyo anatakiwa kuosha tupu ya nyuma kwa maji au kwa mawe.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 22
Imechapishwa: 09/12/2021
https://firqatunnajia.com/11-sharti-kumi-za-wudhuu-ii/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)