Katika kisa hiki kuna mazingatio ikiwa ni pamoja na kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwa mkali kwa mtu huyu, hakumkemea na wala hakumkaripia. Kwa kuwa amekuja hali ya kuwa ni mwenye kutubia na ni mwenye kujuta. Kuna tofauti kati ya mtu mkaidi na ambaye yuko katika hali ya salama aliyekuja akitaka tumsaidie na akituomba tumuokoe na yale aliyotumbukia ndani yake. Ndio maana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alitangamana naye namna hii ambapo alirudi kwa familia yake akiwa na zawadi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambayo ni tende hizi zilizokuwa ni faradhi kwake. Ingelikuwa sio kwa sababu ya umasikini wake basi ingelikuwa ni juu yake kuwalisha masikini sitini.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Dawr-ul-Mar´ah fiy Iswlaah-il-Mujtama´ https://www.sahab.net/home/?p=806
- Imechapishwa: 02/02/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket