70 – Hudhayfah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia:
“Alikuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapotaka kulala husema:
بِاسْـمِكَ اللّهُـمَّ أَمـوتُ وَأَحْـيا
”Kwa jina lako, ee Allaah, ninakufa na ninakuwa hai.”
Na anapoamka kutoka usingizini husema:
الْحَمْدُ للَّهِ الَّذِي أَحْيَانَا بَعْدَ مَا أَمَاتَنَا، وَإِلَيْهِ النُّشُورُ
“Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye ametupa uhai baada ya kutufisha na Kwake ndiko tutafufuliwa.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy.
71 – al-Baraa´ (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapotaka kulala husema:
اللهُمَّ بِاسْمِكَ أحْيَا وَبِاسْمِكَ أُمُوتُ
“Ee Allaah, kwa jina Lako nakuwa hai na kwa jina Lako ninakufa.”
Na anapoamka husema:
الْحَمْدُ للَّهِ الَّذِي أَحْيَانَا بَعْدَ مَا أَمَاتَنَا، وَإِلَيْهِ النُّشُورُ
“Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye ametupa uhai baada ya kutufisha na Kwake ndiko tutafufuliwa.”[2]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Hadiyth hizi mbili zinafahamisha uwekwaji wa Shari´ah ya kusema Dhikr hii wakati wa kulala na wakati wa kuamka. Wakati wa kulala mtu aseme:
اللهُمَّ بِاسْمِكَ أحْيَا وَبِاسْمِكَ أُمُوتُ
“Ee Allaah, kwa jina Lako nakuwa hai na kwa jina Lako ninakufa.”
Maana yake ni kwamba napata uhai na kufa kutokana na jina Lako, ee Allaah, na kutokana na kukutaja.
Wakati wa kuamka aseme:
الْحَمْدُ للَّهِ الَّذِي أَحْيَانَا بَعْدَ مَا أَمَاتَنَا، وَإِلَيْهِ النُّشُورُ
“Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye ametupa uhai baada ya kutufisha na Kwake ndiko tutafufuliwa.”
Ameita kuamka kutoka usingizini uhai na akaita kulala kuwa ni kifo, kwa sababu kulala ni kifo kidogo. Amesema (Ta´ala):
اللَّهُ يَتَوَفَّى الْأَنفُسَ حِينَ مَوْتِهَا وَالَّتِي لَمْ تَمُتْ فِي مَنَامِهَا فَيُمْسِكُ الَّتِي قَضَى عَلَيْهَا الْمَوْتَ وَيُرْسِلُ الْأُخْرَى إِلَى أَجَلٍ مُسَمًّىَ
“Allaah anazifisha nafsi wakati wa kufa kwake na zile zisizokufa katika usingizi wake. Huzizuia zile ambazo amezihukumia mauti na huzituma nyingine mpaka katika muda maalumu uliopangwa.”[3]
[1] al-Bukhaariy (6324).
[2] al-Bukhaariy (6312) na Muslim (2711).
[3] 39:42
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 77-78
- Imechapishwa: 22/10/2025
70 – Hudhayfah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia:
“Alikuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapotaka kulala husema:
بِاسْـمِكَ اللّهُـمَّ أَمـوتُ وَأَحْـيا
”Kwa jina lako, ee Allaah, ninakufa na ninakuwa hai.”
Na anapoamka kutoka usingizini husema:
الْحَمْدُ للَّهِ الَّذِي أَحْيَانَا بَعْدَ مَا أَمَاتَنَا، وَإِلَيْهِ النُّشُورُ
“Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye ametupa uhai baada ya kutufisha na Kwake ndiko tutafufuliwa.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy.
71 – al-Baraa´ (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapotaka kulala husema:
اللهُمَّ بِاسْمِكَ أحْيَا وَبِاسْمِكَ أُمُوتُ
“Ee Allaah, kwa jina Lako nakuwa hai na kwa jina Lako ninakufa.”
Na anapoamka husema:
الْحَمْدُ للَّهِ الَّذِي أَحْيَانَا بَعْدَ مَا أَمَاتَنَا، وَإِلَيْهِ النُّشُورُ
“Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye ametupa uhai baada ya kutufisha na Kwake ndiko tutafufuliwa.”[2]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Hadiyth hizi mbili zinafahamisha uwekwaji wa Shari´ah ya kusema Dhikr hii wakati wa kulala na wakati wa kuamka. Wakati wa kulala mtu aseme:
اللهُمَّ بِاسْمِكَ أحْيَا وَبِاسْمِكَ أُمُوتُ
“Ee Allaah, kwa jina Lako nakuwa hai na kwa jina Lako ninakufa.”
Maana yake ni kwamba napata uhai na kufa kutokana na jina Lako, ee Allaah, na kutokana na kukutaja.
Wakati wa kuamka aseme:
الْحَمْدُ للَّهِ الَّذِي أَحْيَانَا بَعْدَ مَا أَمَاتَنَا، وَإِلَيْهِ النُّشُورُ
“Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye ametupa uhai baada ya kutufisha na Kwake ndiko tutafufuliwa.”
Ameita kuamka kutoka usingizini uhai na akaita kulala kuwa ni kifo, kwa sababu kulala ni kifo kidogo. Amesema (Ta´ala):
اللَّهُ يَتَوَفَّى الْأَنفُسَ حِينَ مَوْتِهَا وَالَّتِي لَمْ تَمُتْ فِي مَنَامِهَا فَيُمْسِكُ الَّتِي قَضَى عَلَيْهَا الْمَوْتَ وَيُرْسِلُ الْأُخْرَى إِلَى أَجَلٍ مُسَمًّىَ
“Allaah anazifisha nafsi wakati wa kufa kwake na zile zisizokufa katika usingizi wake. Huzizuia zile ambazo amezihukumia mauti na huzituma nyingine mpaka katika muda maalumu uliopangwa.”[3]
[1] al-Bukhaariy (6324).
[2] al-Bukhaariy (6312) na Muslim (2711).
[3] 39:42
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 77-78
Imechapishwa: 22/10/2025
https://firqatunnajia.com/11-adhkaar-wakati-wa-kuamka-kutoka-usingizini/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
