109. Kukukusanyika kwa ajili ya kutoa pole na kuandaa chakula

111 – Inapaswa kuepuka mambo mawili japokuwa watu wengi wamezoea kuyafanya:

1 – Kukusanyika kwa ajili ya kutoa pole katika sehemu maalum kama vile nyumbani, makaburini au msikitini.

2 – Familia ya maiti kuandaa chakula kwa ajili ya kuwakaribisha wanaokuja kutoa pole.

Hayo ni kwa sababu ya Hadiyth ya Jariyr bin ´Abdullaah al-Bajaliy (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza:

“Tulikuwa tukizingatia… ”

Imekuja katika upokezi mwingine:

”… tukiona kukusanyika kwa ajili ya kutoa pole kwa familia ya maiti na kuandaa chakula baada ya kumzika kwamba ni katika kuomboleza.”

Ameipokea Ahmad (6905), Ibn Maajah (1/490) na riwaya nyingine pia ni kutoka kwake. Cheni yake ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa masharti al-Bukhaariy na Muslim. Ni Swahiyh kwa mujibu wa an-Nawawiy (5/320) na al-Buuswayriy katika “az-Zawaa-id”.

  • Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz wa Bid´ahaa, uk. 210-211
  • Imechapishwa: 30/07/2026