79 – Ibn Abiy ´Umar ametukhabarisha: Sufyaan ametukhabarisha, kutoka kwa Mis´ar, kutoka kwa Muhaarib, ambaye amesema:

“Tuliitangamana na al-Qaasim bin ‘Abdir-Rahmaan na akatushinda kwa mambo matatu: swalah nyingi, ukimya mrefu na ukarimu.”

80 – Abu Bakr ametukhabarisha: Wakiy´ ametukhabarisha, kutoka kwa Sufyaan, kutoka kwa Thawr, kutoka kwa Sulaym bin ´Aamir, kutoka kwa Abud-Dardaa’, ambaye amesema:

“Kizuizi bora kwa mtu ni nyumbani kwake. Atahifadhi humo ulimi wake na macho yake.”

81 – Ibn Abiy ´Umar ametukhabarisha: Sufyaan ametukhabarisha, kutoka kwa Ibn Abiy Khaalid, kutoka kwa Qays bin Abiy Haazim: Nimemsikia Twalhah bin ´Ubaydillaah, mmoja katika watu wapole wa Quraysh, akisema:

“Aibu ndogo kwa mtu ni kukaa katika nyumba yake.”

82 – Abu Twaalib al-Jurjaaniy ametukhabarisha: Muhammad bin Salamah ametukhabarisha, kutoka kwa Muhammad bin Ishaaq, kutoka kwa Ibn Abiy Najiyh, kutoka kwa Umm Mubashshir bint al-Baraa’ bin Ma´ruur, ambaye amesimulia kuwa amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiwaambia Maswahabah zake:

“Je, nisikujulishe watu ambao ni wabora zaidi?” Wakasema: ”Ndio, ee Mtume wa Allaah.” Akasema: “Mtu anayejikinga na shari za watu.”[1]

83 – Muhammad bin Fudhwayl ametukhabarisha: Husayn bin ´Aliy al-Ju´fiy ametukhabarisha:

“Muhammad bin Nadhwr al-Haarithiy alimwambia Abul-Ahwasw: “Je, si wanadai kwamba Yeye anasema ‘Mimi nakaa na yule mwenye kunitaja Mimi`?” Akasema: “Ndiyo.” Ndipo akasema: “Hakuna mtu anayepaswa kukaa na watu.”

84 – Abul-Waliyd at-Twayaalisiy ametukhabarisha: Shu´bah ametukhabarisha: Khubayb bin ´Abdir-Rahmaan amenikhabarisha: Nimemsikia Hafsw bin ´Aaswim akisema kwamba ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) akisema:

”Chukueni fungu lenu katika kujitenga.”

85 – Abu Bakr ametukhabarisha: Abu Usaamah ametukhabarisha, kutoka kwa Mis´ar, kutoka kwa Wadiy´ah al-Answaariy, ambaye ameeleza kuwa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

”Kujitenga kuna raha kutokana na matangamano maovu.”

86 – Hudbah ametukhabarisha: Haazim al-Qutwa´iy ametukhabarisha, kutoka kwa Maalik bin Diynaar, ambaye amesema:

“Jiepusheni na kila kundi ambalo hufaidiki nalo kheri yoyote.”

87 – Ibn Numayr ametukhabarisha: Abu Salamah ametukhabarisha, kutoka kwa al-A´mash, ambaye amesimulia kwamba ´Umar amesema:

”Raha inapatikana katika kuepuka matangamano maovu.”

88 – Ibraahiym bin Hajjaaj as-Saamiy ametukhabarisha: Salaam bin Abiy Mutwiy´ ametukhabarisha: Nimemsikia Qataadah akisema: ´Umar bin al-Khattwaab amesema:

”Yule anayesuhubiana na mtu muovu hasalimiki.”

[1] Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb” (2737).

  • Muhusika: Imaam Abu Bakr Ahmad bin Abiy ´Aaswim ash-Shaybaaniy (a.f.k. 287)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-uz-Zuhd, uk. 21-22
  • Imechapishwa: 29/06/2025