71 – Duhaym ametukhabarisha: al-Waliyd bin Muslim ametukhabarisha, kutoka kwa al-Awzaa´iy, kutoka kwa az-Zuhriy, kutoka kwa Abu Salamah, kutoka kwa Abu Hurayrah, ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Hazini mwenye kuzini pale anapozini hali ya kuwa ni muumini, na wala haibi mwenye kuiba pale anapoiba hali ya kuwa ni muumini.”[1]

al-Awzaa’iy akasema:

“Nilimuuliza az-Zuhriy: “Ee Abu Bakr, ni Hadiyth gani hiyo?” Akasema: “Ujumbe ni wenye kutoka kwa Allaah, ni jukumu la Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) kufikisha na ni juu yetu kujisalimisha.”

72 – Abu Bakr ametukhabarisha: Abu Usaamah ametukhabarisha: al-´Alaa’ bin ´Abdir-Rahmaan ametukhabarisha:

“Bedui mmoja alitujia na kusema: “Nilihamia Kuufah na nikakutana na Suwayd bin Ghaflah, ambaye alisema: “Natamani ningelikuwa na mwanamke mzuri, kitu cha kuweza kunifanya kuweza kuishi na makazi hapa kandoni kidogo.”

73 – Ibn Abiy ´Umar ametukhabarisha: Sufyaan ametukhabarisha:

“Raqabah aliulizwa kuhusu jambo na akasema: ”Mpaka kupambazuke alfajiri.” Ibn-ul-Mas’uudiy akasema: “Unasemaje ikiwa alfajiri haikupambazuka mpaka nusu ya usiku?” Akasema: ”Lazimiana na kunyamaza, ee mpwa wangu!”

74 – Abu Bakr ametukhabarisha: ´Aliy bin Hafsw ametukhabarisha: Shu´bah ametukhabarisha, kutoka kwa Khubayb bin ´Abdir-Rahmaan, kutoka wa Hafsw bin ´Aaswim, kutoka kwa Abu Hurayrah, ambaye ameeleza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Inatosha kwa mtu kuwa ni dhambi kuzungumzia kila anachokisikia.”[2]

75 – Abu Bakr ametukhabarisha: Ibn Mahdiy ametukhabarisha, kutoka kwa Sufyaan, kutoka kwa Abu Ishaaq, kutoka kwa Abul-Ahwasw, kutoka kwa ´Abdullaah, ambaye amesema:

”Inatosha kwa mtu kuwa mwongo kuzungumzia kila anachokisikia.”

76 – Abu Bakr ametukhabarisha: Yaziyd bin Haaruun ametukhabarisha: Hammaad bin Salamah ametukhabarisha, kutoka kwa Abu Ja´far al-Khatmiy, ambaye ameeleza kwamba babu yake ´Umayr bin Habiyb aliwausia wanawe na kusema:

“Jihadharini na kukaa pamoja na wapumbavu. Kwani hakika kukaa na wapumbavu ni ugonjwa.”

77 – al-Huutwiy ametukhabarisha: Yahyaa bin Swaalih ametukhabarisha, kutoka kwa ´Abdul-Malik bin Mudrik al-Kalaa-iy, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Abud-Dardaa’, ambaye amesema:

“Katika uelewa wa mtu ni pamoja na anatembea, anaingia na anaotoka pamoja na wanazuoni.”

78 – Ibn Numayr ametukhabarisha: Abu Mu´aawiyah na Ibn Fudhayl wametukhabarisha: al-A´mash ametukhabarisha, kutoka kwa ´Umaarah, kutoka kwa Abul-Ahwasw, ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Jizowezeni kheri. Kwani hakika kheri inafanywa kwa kuizowea.”

[1] al-Bukhaariy (2475) na Muslim (57).

[2] Muslim (5) na Abu Daawuud (4992).

  • Muhusika: Imaam Abu Bakr Ahmad bin Abiy ´Aaswim ash-Shaybaaniy (a.f.k. 287)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-uz-Zuhd, uk. 19-20
  • Imechapishwa: 29/06/2025