Sulaymaan at-Taymiy amesema:
”Kama ningeulizwa Allaah yuko wapi, basi ningesema kuwa yupo juu ya mbingu.”
Swahiyh.
Shurayh bin ´Ubayd alikuwa akisema:
”Umeinuka Kwako mlio wa matakaso. Umepanda Kwako utulivu wa utakatifu. Utakasifu ni Wako, ee Mwenye Ukuu. Mikononi Mwako ipo mamlaka, falme, funguo na makadirio.”
Ameipokea Abush-Shaykh.
Wakati Jariyr bin al-Khatwafiy alipotaka kumsifia ´Abdul-Malik bin Marwaan alimwambia:
“Ni nini kilichokuleta, ee Jariyr?” Akasema:
Amenileta kwako Allaah Aliye juu ya ´Arshi Yake
– na nuru na Uislamu vinakushuhudia
Ismaa´iyl bin Abiy Khaalid ameeleza kutoka kwa Abiy ´Iysaa (Rahimahu Allaah) ambaye amesema:
”Wakati Mola alipolingana juu ya Kursiy Yake kuna Malaika mmoja ambaye alisujudu. Hakunyanyua kichwa chake wala hatakinyanyua mpaka Siku ya Qiyaamah. Siku ya Qiyaamah atasema: “Sikukuabudu vile ipasavyo.”
Ameipokea Ibn-ul-Mubaarak katika ”az-Zuhd” na Abush-Shaykh katika ”al-´Adhwamah”.
Mujaahid amesema kuhusiana na maneno Yake (Ta´ala):
وَنَادَيْنَاهُ مِن جَانِبِ الطُّورِ الْأَيْمَنِ وَقَرَّبْنَاهُ نَجِيًّا
”Tukamwita kutoka upande wa kulia wa mlima na Tukamkurubisha kuzungumza naye kwa siri.”[1]
”Baina ya mbingu ya saba na ´Arshi kuna pazia 70.000. Akaendelea kumsogeza karibu Muusa mpaka baina Yake na Muusa kukawa kuna pazia moja tu. Hatimaye alipoona mahali Pake na akasikia uandishi wa kalamu akasema:
رَبِّ أَرِنِي أَنظُرْ إِلَيْكَ
“Mola wangu! Nionyeshe ili nikutazame.”[2][3]
Ameipokea al-Bayhaqiy.
Rabiy´ah amesema:
”Kulingana juu kunatambulika. Namna haitambuliki. Ujumbe ni wenye kutoka kwa Allaah, ni juu ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) kufikisha na ni juu yetu kuamini.”[4]
Muhayswin aliisoma Aayah namna hii:
وَفِي السَّمَاء رازِقُكُم وَمَا تُوعَدُونَ
”Juu ya mbingu yuko Mruzuku Wenu na yale mnayoahidiwa.”[5]
Hammaad bin Zayd amesema:
”Nimemsikia Ayyuub as-Sikhtiyaaniy wakati alipowataja Mu´tazilah: ”´Aqiydah yao inazungukia kusema kwamba hakuna chochote juu ya mbingu.”[6]
Ameipokea at-Twabaaraniy katika ”as-Sunan”.
al-Awzaa´iy amesema:
”Tulikuwa wakati ambao wanafunzi wa Maswahabah wamejaa tukisema: ”Hakika Allaah (Ta´ala) Yuko juu ya ´Arshi Yake na tunaziamini zile sifa Zake zilizopokelewa na Sunnah.”[7]
Ameipokea al-Bayhaqiy katika ”al-Asmaa’ was-Swifaat”.
Na amesema Imaam Muwafaq ad-Diyn: Imenifikia kutoka kwa Abuu Haniyfah – Allaah Amrehemu – kwamba amesema: Mtu yeyote anayekataa kuwa Allaah yuko mbinguni basi amekufuru.
Na amesema Maalik: Allaah yuko mbinguni, na elimu Yake iko kila mahali. Ameipokea…
[1] 19:52
[2] 7:143
[3] Swahiyh kwa mujibu wa adh-Dhahabiy katika “al-´Uluww”, uk. 129, cheni ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Mukhtaswar-ul-´Uluww” (111).
[4] Swahiyh kwa mujibu wa adh-Dhahabiy katika “al-´Uluww”, uk. 128, cheni ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Mukhtaswar-ul-´Uluww” (110).
[5] 51:22
[6] Cheni ya wapokezi iko wazi kama jua na imara zaidi kama nguzo kwa mujibu wa adh-Dhahabiy katika “al-´Uluww”, uk. 129.
[7] al-Albaaniy amesema:
”Ni Swahiyh kwa mujibu wa Ibn Taymiyyah katika ”at-Tadmuriyyah”, na Ibn-ul-Qayyim akaafikiana naye katika “Ijtimaa´-ul-Juyuush al-Islaamiyyah”, uk. 43. Mtunzi amesema katika ufupisho wake kwamba ”Wapokezi wake ni maimamu na wenye kuaminika”.” (Mukhtaswar-ul-´Uluww (121))
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad bin ´Abdil-Haadiy al-Maqdisiy (afk. 744)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Kalaam ´alaa Mas-alat-il-Istiwaa’ ´alaal-´Arsh, uk. 48-50
- Imechapishwa: 21/12/2025
Sulaymaan at-Taymiy amesema:
”Kama ningeulizwa Allaah yuko wapi, basi ningesema kuwa yupo juu ya mbingu.”
Swahiyh.
Shurayh bin ´Ubayd alikuwa akisema:
”Umeinuka Kwako mlio wa matakaso. Umepanda Kwako utulivu wa utakatifu. Utakasifu ni Wako, ee Mwenye Ukuu. Mikononi Mwako ipo mamlaka, falme, funguo na makadirio.”
Ameipokea Abush-Shaykh.
Wakati Jariyr bin al-Khatwafiy alipotaka kumsifia ´Abdul-Malik bin Marwaan alimwambia:
“Ni nini kilichokuleta, ee Jariyr?” Akasema:
Amenileta kwako Allaah Aliye juu ya ´Arshi Yake
– na nuru na Uislamu vinakushuhudia
Ismaa´iyl bin Abiy Khaalid ameeleza kutoka kwa Abiy ´Iysaa (Rahimahu Allaah) ambaye amesema:
”Wakati Mola alipolingana juu ya Kursiy Yake kuna Malaika mmoja ambaye alisujudu. Hakunyanyua kichwa chake wala hatakinyanyua mpaka Siku ya Qiyaamah. Siku ya Qiyaamah atasema: “Sikukuabudu vile ipasavyo.”
Ameipokea Ibn-ul-Mubaarak katika ”az-Zuhd” na Abush-Shaykh katika ”al-´Adhwamah”.
Mujaahid amesema kuhusiana na maneno Yake (Ta´ala):
وَنَادَيْنَاهُ مِن جَانِبِ الطُّورِ الْأَيْمَنِ وَقَرَّبْنَاهُ نَجِيًّا
”Tukamwita kutoka upande wa kulia wa mlima na Tukamkurubisha kuzungumza naye kwa siri.”[1]
”Baina ya mbingu ya saba na ´Arshi kuna pazia 70.000. Akaendelea kumsogeza karibu Muusa mpaka baina Yake na Muusa kukawa kuna pazia moja tu. Hatimaye alipoona mahali Pake na akasikia uandishi wa kalamu akasema:
رَبِّ أَرِنِي أَنظُرْ إِلَيْكَ
“Mola wangu! Nionyeshe ili nikutazame.”[2][3]
Ameipokea al-Bayhaqiy.
Rabiy´ah amesema:
”Kulingana juu kunatambulika. Namna haitambuliki. Ujumbe ni wenye kutoka kwa Allaah, ni juu ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) kufikisha na ni juu yetu kuamini.”[4]
Muhayswin aliisoma Aayah namna hii:
وَفِي السَّمَاء رازِقُكُم وَمَا تُوعَدُونَ
”Juu ya mbingu yuko Mruzuku Wenu na yale mnayoahidiwa.”[5]
Hammaad bin Zayd amesema:
”Nimemsikia Ayyuub as-Sikhtiyaaniy wakati alipowataja Mu´tazilah: ”´Aqiydah yao inazungukia kusema kwamba hakuna chochote juu ya mbingu.”[6]
Ameipokea at-Twabaaraniy katika ”as-Sunan”.
al-Awzaa´iy amesema:
”Tulikuwa wakati ambao wanafunzi wa Maswahabah wamejaa tukisema: ”Hakika Allaah (Ta´ala) Yuko juu ya ´Arshi Yake na tunaziamini zile sifa Zake zilizopokelewa na Sunnah.”[7]
Ameipokea al-Bayhaqiy katika ”al-Asmaa’ was-Swifaat”.
Na amesema Imaam Muwafaq ad-Diyn: Imenifikia kutoka kwa Abuu Haniyfah – Allaah Amrehemu – kwamba amesema: Mtu yeyote anayekataa kuwa Allaah yuko mbinguni basi amekufuru.
Na amesema Maalik: Allaah yuko mbinguni, na elimu Yake iko kila mahali. Ameipokea…
[1] 19:52
[2] 7:143
[3] Swahiyh kwa mujibu wa adh-Dhahabiy katika “al-´Uluww”, uk. 129, cheni ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Mukhtaswar-ul-´Uluww” (111).
[4] Swahiyh kwa mujibu wa adh-Dhahabiy katika “al-´Uluww”, uk. 128, cheni ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Mukhtaswar-ul-´Uluww” (110).
[5] 51:22
[6] Cheni ya wapokezi iko wazi kama jua na imara zaidi kama nguzo kwa mujibu wa adh-Dhahabiy katika “al-´Uluww”, uk. 129.
[7] al-Albaaniy amesema:
”Ni Swahiyh kwa mujibu wa Ibn Taymiyyah katika ”at-Tadmuriyyah”, na Ibn-ul-Qayyim akaafikiana naye katika “Ijtimaa´-ul-Juyuush al-Islaamiyyah”, uk. 43. Mtunzi amesema katika ufupisho wake kwamba ”Wapokezi wake ni maimamu na wenye kuaminika”.” (Mukhtaswar-ul-´Uluww (121))
Muhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad bin ´Abdil-Haadiy al-Maqdisiy (afk. 744)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Kalaam ´alaa Mas-alat-il-Istiwaa’ ´alaal-´Arsh, uk. 48-50
Imechapishwa: 21/12/2025
https://firqatunnajia.com/10-kama-ningeulizwa/