Tofauti kati ya Ahl-us-Sunnah na Ahl-ul-Bid´ah, ni kwamba wanaposikia maelezo kuhusu sifa za Mola basi wanayarudisha papohapo. Hawayakubali. Au…[1] kwa dhahiri kisha baadaye wanayapindisha maana kwa lengo la kuyabatilisha maelezo kuanzia msingi wake, na kubatilisha…[2] akili na maoni yao. Hata hivyo wanajua kwa yakini kabisa ya kwamba yale aliyosema Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndivo kama alivosema. Kwa sababu yeye alikuwa ni mtambuzi zaidi juu ya Mola (Jalla wa ´Alaa) kuliko mwengine yeyote, na hakuna alichosema juu Yake isipokuwa ni haki, kweli na wahy. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَمَا يَنطِقُ عَنِ الْهَوَىٰ إِنْ هُوَ إِلَّا وَحْيٌ يُوحَىٰ
”Hatamki kwa matamanio yake. Hayo ayasemayo si chochote isipokuwa ni Wahy unaofunuliwa kwake.”[3]
Imamu wa maimamu az-Zuhriy na wengineo katika maimamu wengine (Radhiya Allaahu ´anhum) wamesema:
”Ujumbe ni wenye kutoka kwa Allaah, ni jukumu la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kufikisha na jukumu letu ni kujisalimisha.”
Yuunus bin ´Abdis-Swamad bin Ma´qal amesimulia kutoka kwa baba yake aliyesema:
”al-Ja´d bin Dirham alifika kwa Wahb bin Munabbih akimuuliza kuhusu sifa Zake Allaah (Ta´ala), ambapo akasema: ”Maangamivu ni kwako, ee al-Ja´d! Kutokana na baadhi ya mambo hakika mimi nakuzingatia kuwa mwenye kuangamia. Ee al-Ja´d! Endapo Allaah asingetueleza ndani ya Kitabu Chake kwamba yuko na mikono miwili, jicho na uso, basi tusingelisema hivo. Kwa ajili hiyo mche Allaah!” Hapakupita muda mrefu kabla ya al-Ja´d kuuliwa na kusulubiwa[4].
Khaalid bin ´Abdillaah al-Qasriy, ambaye alitoa Khutbah siku ya Adhhwhaa Baswrah, akasema mwishoni mwa Khutbah yake:
“Enyi watu! Chinjeni! Allaah akubali vichinjwa vyenu. Mimi namchinja al-Ja´d bin Dirham. Kwani anadai kwamba Allaah hakumfanya Ibraahiym kuwa kipenzi wa karibu na wala hakuzungumza na Muusa maneno ya kihakika – Allaah ametakasika na kutukuka kutokana na anayoyasema al-Ja´d!”
Baada ya hapo akashuka chini, akamchinja kwa mikono yake na akaamrisha asulubiwe baada ya hapo[5].
[1] Maneno hayako wazi katika maandishi.
[2] Maneno hayako wazi katika maandishi.
[3] 53:3-4
[4] Tazama ”Siyar A´laam-in-Nubalaa’” (5/433).
[5] Tazama ”Siyar A´laam-in-Nubalaa’” (5/433).
- Mhusika: Imaam Abu ´Uthmaan Ismaa´iyl bin ´Abdir-Rahmaan as-Swaabuuniy (afk. 449)
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ´Aqiydat-us-Salaf wa Aswhaab-il-Hadiyth, uk. 189-191
- Imechapishwa: 05/12/2023
Tofauti kati ya Ahl-us-Sunnah na Ahl-ul-Bid´ah, ni kwamba wanaposikia maelezo kuhusu sifa za Mola basi wanayarudisha papohapo. Hawayakubali. Au…[1] kwa dhahiri kisha baadaye wanayapindisha maana kwa lengo la kuyabatilisha maelezo kuanzia msingi wake, na kubatilisha…[2] akili na maoni yao. Hata hivyo wanajua kwa yakini kabisa ya kwamba yale aliyosema Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndivo kama alivosema. Kwa sababu yeye alikuwa ni mtambuzi zaidi juu ya Mola (Jalla wa ´Alaa) kuliko mwengine yeyote, na hakuna alichosema juu Yake isipokuwa ni haki, kweli na wahy. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَمَا يَنطِقُ عَنِ الْهَوَىٰ إِنْ هُوَ إِلَّا وَحْيٌ يُوحَىٰ
”Hatamki kwa matamanio yake. Hayo ayasemayo si chochote isipokuwa ni Wahy unaofunuliwa kwake.”[3]
Imamu wa maimamu az-Zuhriy na wengineo katika maimamu wengine (Radhiya Allaahu ´anhum) wamesema:
”Ujumbe ni wenye kutoka kwa Allaah, ni jukumu la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kufikisha na jukumu letu ni kujisalimisha.”
Yuunus bin ´Abdis-Swamad bin Ma´qal amesimulia kutoka kwa baba yake aliyesema:
”al-Ja´d bin Dirham alifika kwa Wahb bin Munabbih akimuuliza kuhusu sifa Zake Allaah (Ta´ala), ambapo akasema: ”Maangamivu ni kwako, ee al-Ja´d! Kutokana na baadhi ya mambo hakika mimi nakuzingatia kuwa mwenye kuangamia. Ee al-Ja´d! Endapo Allaah asingetueleza ndani ya Kitabu Chake kwamba yuko na mikono miwili, jicho na uso, basi tusingelisema hivo. Kwa ajili hiyo mche Allaah!” Hapakupita muda mrefu kabla ya al-Ja´d kuuliwa na kusulubiwa[4].
Khaalid bin ´Abdillaah al-Qasriy, ambaye alitoa Khutbah siku ya Adhhwhaa Baswrah, akasema mwishoni mwa Khutbah yake:
“Enyi watu! Chinjeni! Allaah akubali vichinjwa vyenu. Mimi namchinja al-Ja´d bin Dirham. Kwani anadai kwamba Allaah hakumfanya Ibraahiym kuwa kipenzi wa karibu na wala hakuzungumza na Muusa maneno ya kihakika – Allaah ametakasika na kutukuka kutokana na anayoyasema al-Ja´d!”
Baada ya hapo akashuka chini, akamchinja kwa mikono yake na akaamrisha asulubiwe baada ya hapo[5].
[1] Maneno hayako wazi katika maandishi.
[2] Maneno hayako wazi katika maandishi.
[3] 53:3-4
[4] Tazama ”Siyar A´laam-in-Nubalaa’” (5/433).
[5] Tazama ”Siyar A´laam-in-Nubalaa’” (5/433).
Mhusika: Imaam Abu ´Uthmaan Ismaa´iyl bin ´Abdir-Rahmaan as-Swaabuuniy (afk. 449)
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: ´Aqiydat-us-Salaf wa Aswhaab-il-Hadiyth, uk. 189-191
Imechapishwa: 05/12/2023
https://firqatunnajia.com/10-ahl-us-sunnah-wanajisalimisha-na-ahl-ul-bidah-wanaasia/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)