09. Hadiyth ”Hakika hawatoacha watu kubaki nyuma hadi Allaah… ”

22 – Abu Sa’iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliona katika Maswahabah zake kusogela nyuma kidogo ambapo akawaambia:

”Sogeeni mbele, nifuateni na wawafuateni wale walioko nyuma yenu. Hakika hawatoacha watu kubaki nyuma hadi Allaah awaache nyuma.”[1]

23 – ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ameeleza ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Hawatoacha watu kuchelewa na safu ya kwanza hadi Allaah awacheleweshe na Moto.”[2]

[1] Muslim (438).

[2] Abu Daawuud (679), Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan (2153) kwa ukaguzi wa al-Albaaniy. Ni nzuri kwa mujibu wa Shaykh Ibn Baz (Rahimahu Allaah) katika “at-Tahqiyq wal-Idhwaah.” Shaykh wetu al-Albaaniy ameona kuwa ni Swahiyh katika “Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (630). Tazama pia “Swahiyh-ut-Targhiyb” (510).

  • Muhusika: ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Wasswaabiy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ujuwb Taswiyat-is-Sufuuf
  • Imechapishwa: 03/02/2025