Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Sharti ya nne ni mtu kuondosha hadathi, nako ni kule kutia wudhuu´ unaojulikana.
MAELEZO
Maneno yake matunzi:
“Sharti ya nne… “
Miongoni mwa sharti za kusihi kwa swalah ni kuondosha hadathi. Nako ni kule kutia wudhuu´ unaojulikana. Kwa msemo mwingine ni lazima mtu atawadhe ili aweze kuswali.
Hadathi ni kitu cha kimaana anachokifanya mtu kikamzuia kuswali, kugusa msahafu, kutufu Ka´bah na kadhalika. Hadathi sio najisi. Najisi inapogusa nguo au mwili inaoshwa na sehemu hiyo panasafika. Hadathi, kama vile kinyesi, mkojo au upepo kutoka kupitia njia ya mbele au ya nyuma, kugusa tupu kwa mkono, kula nyama ya ngamia na mengineyo kama yatavyokuja katika maneno ya mtunzi (Rahimahu Allaah) kuhusu vichenguzi vya wudhuu´.
Mtu akipatwa na kitu katika vile vinavyochengua wudhuu´ ndio huitwa ´hadathi`. Ni lazima aondoshe hadathi hii kwa kutawadha. Hiyo ni sharti miongoni mwa sharti za swalah. Asiyeondosha hadathi ambapo akatawadha, basi ni mwenye hadathi na swalah yake ni batili haisihi.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 17-18
- Imechapishwa: 07/12/2021
Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Sharti ya nne ni mtu kuondosha hadathi, nako ni kule kutia wudhuu´ unaojulikana.
MAELEZO
Maneno yake matunzi:
“Sharti ya nne… “
Miongoni mwa sharti za kusihi kwa swalah ni kuondosha hadathi. Nako ni kule kutia wudhuu´ unaojulikana. Kwa msemo mwingine ni lazima mtu atawadhe ili aweze kuswali.
Hadathi ni kitu cha kimaana anachokifanya mtu kikamzuia kuswali, kugusa msahafu, kutufu Ka´bah na kadhalika. Hadathi sio najisi. Najisi inapogusa nguo au mwili inaoshwa na sehemu hiyo panasafika. Hadathi, kama vile kinyesi, mkojo au upepo kutoka kupitia njia ya mbele au ya nyuma, kugusa tupu kwa mkono, kula nyama ya ngamia na mengineyo kama yatavyokuja katika maneno ya mtunzi (Rahimahu Allaah) kuhusu vichenguzi vya wudhuu´.
Mtu akipatwa na kitu katika vile vinavyochengua wudhuu´ ndio huitwa ´hadathi`. Ni lazima aondoshe hadathi hii kwa kutawadha. Hiyo ni sharti miongoni mwa sharti za swalah. Asiyeondosha hadathi ambapo akatawadha, basi ni mwenye hadathi na swalah yake ni batili haisihi.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 17-18
Imechapishwa: 07/12/2021
https://firqatunnajia.com/08-sharti-ya-nne-ya-swalah-kuondosha-hadathi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)