37 – Abu Dardaa´ (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:
“Hakuna muislamu anayemuombea du´aa ndugu yake nyuma ya mgongo wake isipokuwa Malaika husema: “Nawe upewe mfano wake.”
Imekuja katika upokezi mwingine:
“Du´aa ya muislamu kumuombea ndugu yake nyuma ya mgongo wake ni yenye kuitikiwa. Karibu na kichwa chake kuna Malaika aliyepewa kazi ambaye kila anapomuombea du´aa ndugu yake jambo la kheri, Malaika huyo aliyepewa kazi husema: “Aamiyn, nawe upewe mfano wake.”[1]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Hadiyth inafahamisha ubora wa muislamu kumuombea du´aa ndugu yake nyuma ya mgongo wake. Kwa maana nyingine akiwa mbali naye. Du´aa hiyo ni yenye kuitikiwa.
Hadiyth inajulisha pia kuwa ananufaika yule mwombaji na yule mwombewaji, kwa sababu Malaika huitikia “Aamiyn” juu ya du´aa ya mwombaji kwa kusema “Nawe upewe mfano wake”. Hivyo anapewa mfano wa yale aliyomuombea ndugu yake nyuma ya mgongo wake.
[1] Muslim (2732) na (2733).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 41
- Imechapishwa: 08/10/2025
37 – Abu Dardaa´ (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:
“Hakuna muislamu anayemuombea du´aa ndugu yake nyuma ya mgongo wake isipokuwa Malaika husema: “Nawe upewe mfano wake.”
Imekuja katika upokezi mwingine:
“Du´aa ya muislamu kumuombea ndugu yake nyuma ya mgongo wake ni yenye kuitikiwa. Karibu na kichwa chake kuna Malaika aliyepewa kazi ambaye kila anapomuombea du´aa ndugu yake jambo la kheri, Malaika huyo aliyepewa kazi husema: “Aamiyn, nawe upewe mfano wake.”[1]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Hadiyth inafahamisha ubora wa muislamu kumuombea du´aa ndugu yake nyuma ya mgongo wake. Kwa maana nyingine akiwa mbali naye. Du´aa hiyo ni yenye kuitikiwa.
Hadiyth inajulisha pia kuwa ananufaika yule mwombaji na yule mwombewaji, kwa sababu Malaika huitikia “Aamiyn” juu ya du´aa ya mwombaji kwa kusema “Nawe upewe mfano wake”. Hivyo anapewa mfano wa yale aliyomuombea ndugu yake nyuma ya mgongo wake.
[1] Muslim (2732) na (2733).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 41
Imechapishwa: 08/10/2025
https://firqatunnajia.com/07-fadhilah-za-kuomuombea-duaa-nduguyo-nyuma-ya-mgongo-wake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket