Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
19 – Kwa sababu Yeye juu ya kila jambo ni muweza. Kila kitu ni chenye kumuhitajia Yeye. Kila jambo Kwake ni jepesi:
لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖوَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ
“Hakuna chochote kinachofanana Naye – Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.”[1]
MAELEZO
Baadhi wanasema kuwa Allaah ni muweza kwa yale Anayoyataka. Hayo si sahihi. Sahihi ni yale yaliyotajwa katika Qur-aan na Sunnah; kwamba Yeye juu ya kila kitu ni muweza kwa sababu matakwa na uwezo Wake ni vyenye kuenea.
Mu´tazilah wanasema kuwa Allaah (Ta´ala) hakutaka mja aingie ndani ya madhambi; bali mja mwenyewe ndiye kataka hivo, na si Allaah. Kwa ajili hiyo amesema mmoja katika wapotofu wao:
Amedai mjinga na yule mwenye kuonelea kama yeye
ya kwamba Muumba ndiye kahukumu maasi
ikiwa hayo anayoyasema ni kweli
ni kwa nini basi aadhibiwe mzinzi na mwizi akatwe mkono?
Abul-Khattwaab (Rahimahu Allaah) amesema pindi alipokuwa akibainisha haki na usawa:
Wamesema: “Vipi basi matendo ya waja?”
Nikasema hakuna Muumba isipokuwa Mungu mtukufu
Wakasema: “Je, anataka kutokee kwa mambo mabaya?”
Nikasema matakwa yote yanayokana na Mola
Ni upungufu ikiwa yatatokea pasi na kutaka Kwake
Ametakasika kushindwa na kitu duni
Matakwa anayozungumzia Abul-Khattwaab ni ya kilimwengu, na si ya kidini. Hayo atakuja kubainishwa huko mbele.
[1] 42:11
- Mhusika: ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-´Aziyz bin Maaniy´
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Haashiyah ´alaa al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 23-24
- Imechapishwa: 11/11/2021
Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
19 – Kwa sababu Yeye juu ya kila jambo ni muweza. Kila kitu ni chenye kumuhitajia Yeye. Kila jambo Kwake ni jepesi:
لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖوَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ
“Hakuna chochote kinachofanana Naye – Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.”[1]
MAELEZO
Baadhi wanasema kuwa Allaah ni muweza kwa yale Anayoyataka. Hayo si sahihi. Sahihi ni yale yaliyotajwa katika Qur-aan na Sunnah; kwamba Yeye juu ya kila kitu ni muweza kwa sababu matakwa na uwezo Wake ni vyenye kuenea.
Mu´tazilah wanasema kuwa Allaah (Ta´ala) hakutaka mja aingie ndani ya madhambi; bali mja mwenyewe ndiye kataka hivo, na si Allaah. Kwa ajili hiyo amesema mmoja katika wapotofu wao:
Amedai mjinga na yule mwenye kuonelea kama yeye
ya kwamba Muumba ndiye kahukumu maasi
ikiwa hayo anayoyasema ni kweli
ni kwa nini basi aadhibiwe mzinzi na mwizi akatwe mkono?
Abul-Khattwaab (Rahimahu Allaah) amesema pindi alipokuwa akibainisha haki na usawa:
Wamesema: “Vipi basi matendo ya waja?”
Nikasema hakuna Muumba isipokuwa Mungu mtukufu
Wakasema: “Je, anataka kutokee kwa mambo mabaya?”
Nikasema matakwa yote yanayokana na Mola
Ni upungufu ikiwa yatatokea pasi na kutaka Kwake
Ametakasika kushindwa na kitu duni
Matakwa anayozungumzia Abul-Khattwaab ni ya kilimwengu, na si ya kidini. Hayo atakuja kubainishwa huko mbele.
[1] 42:11
Mhusika: ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-´Aziyz bin Maaniy´
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Haashiyah ´alaa al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 23-24
Imechapishwa: 11/11/2021
https://firqatunnajia.com/07-allaah-ni-muweza-wa-kila-kitu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)