2 – Kipengele cha pili: Sifa za Allaah zimegawanyika aina mbili:
1 – Zilizothibitishwa (Thubuutiyyah).
2 – Zilizokanushwa (Salbiyyah).
Zinazothibitishwa ni zile ambazo Allaah amejithibitishia nazo. Mfano wa sifa hizo ni uhai, ujuzi na uwezo. Ni lazima kumthibitishia nazo Allaah kwa njia inayomstahikia. Allaah ndiye ambaye amejithibitishia nazo na Yeye ni mtambuzi zaidi wa sifa Zake.
Zilizokanushwa ni zile ambazo Allaah amejikanushia nazo. Mfano wa sifa hizo ni kudhulumu. Hivyo inalazimika kumkanushia nazo Allaah kwa sababu Allaah amejikanushia nazo. Lakini ni lazima kwa mtu aamini kumthibitishia Allaah kinyume chake kwa njia kamilifu zaidi. Kukanusha hakukuwi kamili mpaka ndani yake kuwemo na jambo la kuthibitisha. Mfano wa hilo ni maneno Yake (Ta´ala):
وَلَا يَظْلِمُ رَبُّكَ أَحَدًا
“Na Mola wako Hamdhulumu yeyote.”[1]
Kwa hivyo ni lazima kumkanushia Allaah kudhulumu sambamba na kuamini kuthibiti uadilifu kwa Allaah kwa njia kamilifu zaidi.
[1] 18:49
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 25
- Imechapishwa: 09/10/2022
2 – Kipengele cha pili: Sifa za Allaah zimegawanyika aina mbili:
1 – Zilizothibitishwa (Thubuutiyyah).
2 – Zilizokanushwa (Salbiyyah).
Zinazothibitishwa ni zile ambazo Allaah amejithibitishia nazo. Mfano wa sifa hizo ni uhai, ujuzi na uwezo. Ni lazima kumthibitishia nazo Allaah kwa njia inayomstahikia. Allaah ndiye ambaye amejithibitishia nazo na Yeye ni mtambuzi zaidi wa sifa Zake.
Zilizokanushwa ni zile ambazo Allaah amejikanushia nazo. Mfano wa sifa hizo ni kudhulumu. Hivyo inalazimika kumkanushia nazo Allaah kwa sababu Allaah amejikanushia nazo. Lakini ni lazima kwa mtu aamini kumthibitishia Allaah kinyume chake kwa njia kamilifu zaidi. Kukanusha hakukuwi kamili mpaka ndani yake kuwemo na jambo la kuthibitisha. Mfano wa hilo ni maneno Yake (Ta´ala):
وَلَا يَظْلِمُ رَبُّكَ أَحَدًا
“Na Mola wako Hamdhulumu yeyote.”[1]
Kwa hivyo ni lazima kumkanushia Allaah kudhulumu sambamba na kuamini kuthibiti uadilifu kwa Allaah kwa njia kamilifu zaidi.
[1] 18:49
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 25
Imechapishwa: 09/10/2022
https://firqatunnajia.com/06-sifa-za-allaah-ni-kwa-njia-ya-kuthibitisha-na-kukanushwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)