Haafidhw ´Abdul-Ghaniy al-Maqdisiy al-Hanbaliy (Rahimahu Allaah) ameema:
185 – ´Abdullaah bin ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesimulia kuwa amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:
“Mkiuona fungeni na mkiuona fungueni. Mkifunikwa na mawingu basi ikadirieni.”[1]
MAELEZO
Hadiyth hii inaeleza kuwa watu wanafunga Ramadhaan kwa kuona mwezi mwandamo. Hadiyth nyingine inasema:
“Mkiona basi fungeni, na mkiona basi fungulieni. Ikiwa imefichika kwenu basi kamilisheni siku thelathini.”[2]
Imekuja katika tamko jengine:
“Fungeni kwa kuonekana kwake na fungueni kwa kuonekana kwake. Ikiwa imefichika kwenu basi kamilisheni hesabu ya Sha’baan kuwa siku thelathini.”[3]
Kwa maana ya kwamba kamilisheni mwezi wa Sha’baan siku thelathini ikiwa mwezi mwandamo haukuonekana kutokana na mawingu au wingu zito.
[1] al-Bukhaariy (1900) na Muslim (1080).
[2] Muslim (1081).
[3] al-Bukhaariy (1909).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Taysiyr Dhil-In´am bisharh ´Umdat-il-Ahkaam (01/436)
- Imechapishwa: 16/02/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)