Maamrisho yamegawanyika aina mbili.
1 – Maamrisho ya uwajibu.
2 – Maamrisho ya kupendeza.
Maamrisho ya uwajibu ni kama vile swalah. Kwa kuwa swalah ni wajibu. Maamrisho ya kupendeza ni kama kutumia Siwaak. Inapendeza.
Makatazo yamegawanyika aina mbili:
1 – Makatazo ya uharamu. Kwa mfano makatazo ya uzinzi.
2 – Makatatazo ya kuchukiza. Ni kama mfano wa makatazo ya mazungumzo baada ya swalah ya ´Ishaa.
Ni mamoja matendo hayo ni ya dhahiri, kama mfano wa swalah na swawm; au yawe yamejificha, kama mfano wa nia, kumtakasia nia Allaah, ukweli na mapenzi. Vivyo hivyo makatazo ni mamoja yawe ya dhahiri, kama mfano wa uzinzi; au yaliyojificha, kama mfano wa majivuno, kiburi, kujionyesha, vifundo, chuki na hasadi. Yote hayo yamekatazwa na hivyo mtu anatakiwa kuyaacha.
Kwa hivyo ´ibaadah imekusanya maamrisho na makatazo ya maneno na matendo, ni mamoja yenye kuonekana na yaliyojificha ambayo yametajwa na Shari´ah. Mtu akifanya aina moja wapo miongoni mwa ´ibaadah hizi akamfanyia asiyekuwa Allaah, basi ametumbukia katika shirki.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tabswiyr-ul-Anaam bisharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 15
- Imechapishwa: 09/04/2023
Maamrisho yamegawanyika aina mbili.
1 – Maamrisho ya uwajibu.
2 – Maamrisho ya kupendeza.
Maamrisho ya uwajibu ni kama vile swalah. Kwa kuwa swalah ni wajibu. Maamrisho ya kupendeza ni kama kutumia Siwaak. Inapendeza.
Makatazo yamegawanyika aina mbili:
1 – Makatazo ya uharamu. Kwa mfano makatazo ya uzinzi.
2 – Makatatazo ya kuchukiza. Ni kama mfano wa makatazo ya mazungumzo baada ya swalah ya ´Ishaa.
Ni mamoja matendo hayo ni ya dhahiri, kama mfano wa swalah na swawm; au yawe yamejificha, kama mfano wa nia, kumtakasia nia Allaah, ukweli na mapenzi. Vivyo hivyo makatazo ni mamoja yawe ya dhahiri, kama mfano wa uzinzi; au yaliyojificha, kama mfano wa majivuno, kiburi, kujionyesha, vifundo, chuki na hasadi. Yote hayo yamekatazwa na hivyo mtu anatakiwa kuyaacha.
Kwa hivyo ´ibaadah imekusanya maamrisho na makatazo ya maneno na matendo, ni mamoja yenye kuonekana na yaliyojificha ambayo yametajwa na Shari´ah. Mtu akifanya aina moja wapo miongoni mwa ´ibaadah hizi akamfanyia asiyekuwa Allaah, basi ametumbukia katika shirki.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tabswiyr-ul-Anaam bisharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 15
Imechapishwa: 09/04/2023
https://firqatunnajia.com/05-aina-mbili-za-maamrisho-na-makatazo/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)