3- Sifa ya tatu: Allaah kila siku anampambia Pepo Yake na anasema:

”Waja wangu wema wanakaribia kuondolewa matatizo na maudhi na kuja Kwangu.”

Allaah (Ta´ala) kila siku anampambia Pepo Yake kwa ajili ya kuwaandalia nayo waja Wake  wema na kuwavutia kuweza kuifikia na anasema (Subhaanah):

”Waja wangu wema wanakaribia kuondolewa matatizo na maudhi na kuja Kwangu.”

Bi maana matatizo ya dunia, tabu na maudhi yake. Anawahimiza katika matendo mema ambayo kwayo ndio kuna kufaulu duniani na Aakhirah na kuifikia Pepo Yake.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majaalis Shahr Ramadhwaan, uk. 10
  • Imechapishwa: 02/04/2020