Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:

6 – Haangamii wala hatoweki.

7 – Wala hakuna kinachokuwa isipokuwa yale ayatakayo.

8 – Mawazo hayawezi kumfikia, fahamu haziwezi kumzunguka Yeye.

9 – Hafanani na viumbe/watu.

MAELEZO

Jumla hizi zinawaraddi Mushabbihah wanaomfananisha Muumba (Subhnaanahu wa Ta´ala) na viumbe. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:

لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖوَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ

“Hakuna chochote kinachofanana Naye – Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.”[1]

Makusudio sio kupinga sifa za Allaah, kama wanavosema Ahl-ul-Bid´ah. Miongoni mwa maneno Abu Haniyfah (Rahimahu Allaah) katika ”Fiqh-ul-Akbar” ni kwamba amesema:

”Hafanani na chochote katika viumbe Wake.”

Kisha akasema (Rahimahu Allaah) baada ya hapo:

”Sifa Zake zote zinazotofautiana na sifa za viumbe. Anajua, lakini sio kama kujua kwetu. Anaweza, lakini sio kama kuweza kwetu. Anaona, lakini sio kama kuona kwetu.”

[1] 42:11

  • Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah – Sharh wa Ta´liyq, uk. 12-13
  • Imechapishwa: 12/09/2024