9 – Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ziwekeni sawa safu zenu, linganisheni mabega yenu, fanyeni wepesi kwa ndugu zenu na zibeni mapengo, kwani hakika kwa shaytwaan huingia kati yenu kama watoto wadogo wa kondoo.”[1]
10 – ´Abdullaah bin ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Zisawazisheni safu, linganisheni mabega, zibeni mapengo, fanyeni wepesi kwa ndugu zenu na msimuachie nafasi kwa shaytwaan. Yeyote atakayeunga safu, basi Allaah atamuunga, na yeyote anayevunja safu, basi Allaah atamvunja.”[2]
11 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wekeni safu sawa katika swalah, kwani hakika kuweka safu sawa ni katika uzuri wa swalah.”[3]
12 – Anas bin Malik (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ziwekeni safu sawa, kwani nawaona nyuma ya mgongo wangu.”
Imekuja katika tamo jengine:
”Swalah ilikimiwa ambapo na Mtume wa Allaah (Swalla Allahu ´alayhi wa sallam) akatugeukia na kusema:
“Ziwekeni safu zenu sawa na simameni karibu pamoja, kwani kwani nawaona nyuma ya mgongo wangu.”[4]
13 – Abu Muusa (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Swalah inapokimiwa, basi zisawazisheni safu zenu…”[5]
14 – Jaabir bin ´Abdillaah al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika katika utimilifu wa swalah ni kule kusawazisha safu.”[6]
[1] Imaam Ahmad (36/597) nr. (22263).
Shaykh Shu’ayb amesema:
“Ni Swahiyh kupitia zingine.”
Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ut-Targhiyb” (1/330).
[2] Ahmad na Abu Daawuud (666). an-Nasaa´iy na Ibn Khuzaymah wamepokea sehemu yake ya mwisho. Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ut-Targhiyb” (495) na ”Swahiyh Abiy Daawuud” (620). al-Mundhiriy amesema:
”Nafasi (الفُرُجَات) ni wingi wa nafasi (فُرْجَه), nayo ni nafasi iliyo wazi kati ya watu wawili.
[3] al-Bukhaariy (689), Muslim (435) na Ibn Hibbaan (2174) kwa ukaguzi wa wa al-Albaaniy.
[4] al-Bukhaariy (687, 686) na Muslim (434).
Lafudhi yake kwa Muslim:
“Kamilisheni safu zenu…”
al-Bukhaariy (692) ameongeza:
“Mmoja wetu alikuwa akiegemeza bega lake na bega la mwenzake na mguu wake na mguu wa mwenzake.” (as-Silsilah as-Swahiyhah (31) ).
[5] Imekuja kwa Muslim (404) kwa lafudhi:
“Mnaposwali, basi simamisheni safu zenu.”
Ibn Hibbaan nr. (2167), (5/540) kwa ukaguzi wa Shu’ayb.
Ibn Khuzaymah (1584), Ahmad Abu ´Awaanah na at-Twayaalisiy.
Ni Swahiyh kwa mujibu wa Shaykh al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) katika maelezo yake ya “Swahiyh Ibn Hibbaan” (2164).
[6] Ahmad (14494), Abu Ya’laa (2168) na at-Twabaraaniy katika “al-Kabiyr” (1744), ´Abdur-Razzaaq katika “al-Muswannaf” (2425).
Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh-ul-Jaamiy’” (2221).
- Muhusika: ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Wasswaabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ujuwb Taswiyat-is-Sufuuf
- Imechapishwa: 15/01/2025
9 – Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ziwekeni sawa safu zenu, linganisheni mabega yenu, fanyeni wepesi kwa ndugu zenu na zibeni mapengo, kwani hakika kwa shaytwaan huingia kati yenu kama watoto wadogo wa kondoo.”[1]
10 – ´Abdullaah bin ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Zisawazisheni safu, linganisheni mabega, zibeni mapengo, fanyeni wepesi kwa ndugu zenu na msimuachie nafasi kwa shaytwaan. Yeyote atakayeunga safu, basi Allaah atamuunga, na yeyote anayevunja safu, basi Allaah atamvunja.”[2]
11 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wekeni safu sawa katika swalah, kwani hakika kuweka safu sawa ni katika uzuri wa swalah.”[3]
12 – Anas bin Malik (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ziwekeni safu sawa, kwani nawaona nyuma ya mgongo wangu.”
Imekuja katika tamo jengine:
”Swalah ilikimiwa ambapo na Mtume wa Allaah (Swalla Allahu ´alayhi wa sallam) akatugeukia na kusema:
“Ziwekeni safu zenu sawa na simameni karibu pamoja, kwani kwani nawaona nyuma ya mgongo wangu.”[4]
13 – Abu Muusa (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Swalah inapokimiwa, basi zisawazisheni safu zenu…”[5]
14 – Jaabir bin ´Abdillaah al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika katika utimilifu wa swalah ni kule kusawazisha safu.”[6]
[1] Imaam Ahmad (36/597) nr. (22263).
Shaykh Shu’ayb amesema:
“Ni Swahiyh kupitia zingine.”
Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ut-Targhiyb” (1/330).
[2] Ahmad na Abu Daawuud (666). an-Nasaa´iy na Ibn Khuzaymah wamepokea sehemu yake ya mwisho. Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ut-Targhiyb” (495) na ”Swahiyh Abiy Daawuud” (620). al-Mundhiriy amesema:
”Nafasi (الفُرُجَات) ni wingi wa nafasi (فُرْجَه), nayo ni nafasi iliyo wazi kati ya watu wawili.
[3] al-Bukhaariy (689), Muslim (435) na Ibn Hibbaan (2174) kwa ukaguzi wa wa al-Albaaniy.
[4] al-Bukhaariy (687, 686) na Muslim (434).
Lafudhi yake kwa Muslim:
“Kamilisheni safu zenu…”
al-Bukhaariy (692) ameongeza:
“Mmoja wetu alikuwa akiegemeza bega lake na bega la mwenzake na mguu wake na mguu wa mwenzake.” (as-Silsilah as-Swahiyhah (31) ).
[5] Imekuja kwa Muslim (404) kwa lafudhi:
“Mnaposwali, basi simamisheni safu zenu.”
Ibn Hibbaan nr. (2167), (5/540) kwa ukaguzi wa Shu’ayb.
Ibn Khuzaymah (1584), Ahmad Abu ´Awaanah na at-Twayaalisiy.
Ni Swahiyh kwa mujibu wa Shaykh al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) katika maelezo yake ya “Swahiyh Ibn Hibbaan” (2164).
[6] Ahmad (14494), Abu Ya’laa (2168) na at-Twabaraaniy katika “al-Kabiyr” (1744), ´Abdur-Razzaaq katika “al-Muswannaf” (2425).
Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh-ul-Jaamiy’” (2221).
Muhusika: ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Wasswaabiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ujuwb Taswiyat-is-Sufuuf
Imechapishwa: 15/01/2025
https://firqatunnajia.com/04-hadiyth-ziwekeni-sawa-safu-zenu-linganisheni-mabega-yenu-fanyeni-wepesi-kwa-ndugu-zenu-na-zibeni-mapengo/