04. Hadiyth “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametuamrisha kujenga misikiti… “

279 – ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:

أمرنا رسولُ الله – صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ – ببناءِ المساجد في الدُّورِ ، وأن تُنَظَّفَ وتُطَيِّبَ

“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametuamrisha kujenga misikiti katika makabila na tuisafisha na kuitia manukato[1].”[2]

Ameipokea Ahmad, Abu Daawuud, Ibn Maajah na Ibn Khuzaymah katika ”as-Swahiyh”. at-Tirmidhiy ameipokea kwa cheni ya wapokezi ilioungana na kwa cheni ya wapokezi inayokosa Swahabah na akasema kuhusu ule upokezi unaokosa Swahabah katika cheni ya wapokezi:

“Hii ni sahihi zaidi.”

[1] Kwa sababu Malaika watukufu wanahudhuria.

[2] Swahiyh.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/231)
  • Imechapishwa: 25/10/2022
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy