03. Kufanya romantiki na mke mchana wa Ramadhaan

Swali: Mwanamme akimbusu mke wache mchana wa Ramadhaan au akafanya naye romantiki funga yake inaharibika?

Jibu: Mwanamme kumbusu mke wake na akafanya naye romantiki pasi na kufanya naye jimaa – na wakati huohuo amefunga – yote hayo yanafaa na hakuna ubaya. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akibusu ilihali amefunga na akichanganyikana nao ilikuwa amefunga. Lakini akichelea kutumbukia katika yale ambayo Allaah amemuharamishia kwa njia ya kwamba ni mwenye matamanio ya haraka, basi itachukizwa kwake kufanya hivo. Akitokwa na manii basi itamlazimu kujizuia na kulipa siku hiyo. Kikosi cha wanachuoni wengi wanaona kuwa hahitajii kutoa kafara. Kwa sababu msingi ni usalama na kutobadilika swawm yake. Jengine ni kwamba ni vigumu kujiepusha na jambo hilo.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ashyaa´ laa tufsid-is-Swawm, uk. 05
  • Imechapishwa: 29/03/2021