Swali 03: Je, ni jambo limewekwa katika Shari´ah kuhudhuria mbele ya kafiri anayetaka kukata roho na kumtamkisha shahaadah[1]?
Jibu: Ni jambo limewekwa katika Shari´ah kama kuna wepesi wa kufanya hivo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa na mfanyakazi wa kiyahudi ambapo siku moja akagonjweka. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaenda kumtembelea na akamtamkisha shahaadah na kumwambia:
“Sema ´hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah`. Myahudi yule akawatazama wazazi wawili ambapo akamwambia: “Mtii Abul-Qaasim! akalitamka.” Ndipo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye amemwokoa kutokamana na Moto.”
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/94).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 12
- Imechapishwa: 10/12/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket