03. Hadiyth “Yule ambaye anamwamini Allaah na siku ya Mwisho katika wanawake zenu… “

166 – Abu Ayyuub al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Yule ambaye anamwamini Allaah na siku ya Mwisho basi amkirimu jirani yake. Yule ambaye anamwamini Allaah na siku ya Mwisho basi asiingie bafu za nje isipokuwa awe na shuka ya juu. Yule ambaye anamwamini Allaah na siku ya Mwisho basi aseme yaliyo mema au anyamaze. Yule ambaye anamwamini Allaah na siku ya Mwisho katika wanawake zenu basi asiingie katika bafu za nje.”[1]

[1] Swahiyh.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/180)
  • Imechapishwa: 05/04/2021
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy