2- Hudhayfah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

“Kuna mtu mmoja aliuliza zama za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo watu wakashikamana tena. Kisha bwana mmoja akampa nao watu wakampa. Ndipo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Yeyote mwenye kuweka msingi mzuri ambapo akaigilizwa, basi atapata ujira wake na mfano wa ujira wa atakayemfuata pasi na kupungua chochote katika ujira wao. Na yeyote mwenye kuweka msingi mbaya ambapo akaigilizwa, basi atapata fungu la dhambi zake na dhambi za atakayemfuata pasi na kupungua chochote katika dhambi zao.”[1]

Ameipokea Ahmad na al-Haakim ambaye amesema:

“Cheni ya wapokezi wake ni Swahiyh.”

3- Ibn Maajah ameipokea kutoka kwa Abu Hurayrah[2].

[1] Nzuri na Swahiyh.

[2] Huu ni upungufu wa wazi, kwa sababu ameipokea Muslim pia (08/62).

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/134)
  • Imechapishwa: 29/04/2020
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy