203 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
لا صلاةَ لِمَنْ لا وُضُوءَ له، ولا وُضُوءَ لِمَنْ لم يَذكُرِ اسمَ اللهِ عليهِ
“Hana swalah ambaye hana wudhuu´, na wala hana wudhuu´ yule ambaye hakutaja jina la Allaah kabla yake.”[1]
Ameipokea Ahmad, Abu Daawuud, Ibn Maajah, at-Twabaraaniy na al-Haakim ambaye amesema:
“Cheni ya wapokezi ni Swahiyh.”
Mambo si kama alivosema, kwa sababu wameisimulia kupitia kwa Ya´quub bin Salamah al-Laythiy, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Abu Hurayrah. al-Bukhaariy na wengine wamesema:
“Haitambuliki kuwa Salamah alisikia kutoka kwa Abu Hurayrah wala Ya´quub kusikia kutoka kwa baba yake.”
Abu Salamah pia hatambuliki na hakun waliyosimulia kutoka kwake isipokuwa mwanawe Ya´quub. Zipo wapi basi sharti za kusihi?
[1] Nzuri kupitia zingine.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/200)
- Imechapishwa: 03/01/2024
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)