31 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mja anakuwa karibu zaidi na Mola wake anapokuwa amesujudu. Hivyo basi, ombeni du´aa kwa wingi.”[1]
Ameipokea Muslim.
32 – Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ama katika Sujuud jitahidini katika du´aa. Kuna matumaini makubwa na nyinyi kuitikiwa.”[2]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Hadiyth hizi mbili zinafahamisha kuwa inapendeza kuomba du´aa kwa wingi katika sujuud. Mja anakuwa karibu zaidi na Mola wake wakati amesujudu. Kwa ajili hiyo amesema (Subhaanah):
وَاسْجُدْ وَاقْتَرِب
”Basi sujudu na kurubia.”[3]
Kwa sababu mja anapiga uso wake, paji la uso na pua yake kwenye udongo juu ya ardhi. Hili hafanyiwi mwingine isipokuwa tu Yeye (Subhaanah). Ndio maana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema:
“Ama katika Sujuud jitahidini katika du´aa. Kuna matumaini makubwa na nyinyi kuitikiwa.”
Bi maana kuna uhakika mkubwa wa nyinyi kuitikiwa.
[1] Muslim (482).
[2] Muslim (479).
[3] 96:19
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 37
- Imechapishwa: 07/10/2025
31 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mja anakuwa karibu zaidi na Mola wake anapokuwa amesujudu. Hivyo basi, ombeni du´aa kwa wingi.”[1]
Ameipokea Muslim.
32 – Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ama katika Sujuud jitahidini katika du´aa. Kuna matumaini makubwa na nyinyi kuitikiwa.”[2]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Hadiyth hizi mbili zinafahamisha kuwa inapendeza kuomba du´aa kwa wingi katika sujuud. Mja anakuwa karibu zaidi na Mola wake wakati amesujudu. Kwa ajili hiyo amesema (Subhaanah):
وَاسْجُدْ وَاقْتَرِب
”Basi sujudu na kurubia.”[3]
Kwa sababu mja anapiga uso wake, paji la uso na pua yake kwenye udongo juu ya ardhi. Hili hafanyiwi mwingine isipokuwa tu Yeye (Subhaanah). Ndio maana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema:
“Ama katika Sujuud jitahidini katika du´aa. Kuna matumaini makubwa na nyinyi kuitikiwa.”
Bi maana kuna uhakika mkubwa wa nyinyi kuitikiwa.
[1] Muslim (482).
[2] Muslim (479).
[3] 96:19
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 37
Imechapishwa: 07/10/2025
https://firqatunnajia.com/02-duaa-za-kwenye-sujuud/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket