56 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alinipa kazi ya kuchunga zakaah ya Ramadhaan. Nikajiliwa na mwenye kuja na kuanza kuchukua chakula ambapo nikamkamata na kumwambia: “Nitakupeleka kwa Mtume wa Allaah…. Akamwambia: “Unapoenda kulala mwako, basi soma Aayaah al-Kursiy. Utaendelea kuhifadhiwa na Allaah na hutokaribiwa na shaytwaan mpaka kupambazuke. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema:
“Amesema kweli ijapo ni mwongo. Huyo alikuwa ni shaytwaan.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy.
MAELEZO
Hadiyth hii inafahamisha kuwa ni jambo limewekwa katika Shari´ah kusoma Aayah al-Kursiy wakati wa kulala na kwamba ni miongoni mwa sababu za Allaah (´Azza wa Jall) kumuhifadhi mja kutokana na shaytwaan.
Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Utaendelea kuhifadhiwa na Allaah… “
Haya ni maneno ya shaytwaan. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akayakubali na kusema:
“Amesema kweli ijapo ni mwongo. Huyo alikuwa ni shaytwaan.”
Hukumu inachukuliwa baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumsadikisha.
[1] al-Bukhaariy (3275).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 66-67
- Imechapishwa: 20/10/2025
56 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alinipa kazi ya kuchunga zakaah ya Ramadhaan. Nikajiliwa na mwenye kuja na kuanza kuchukua chakula ambapo nikamkamata na kumwambia: “Nitakupeleka kwa Mtume wa Allaah…. Akamwambia: “Unapoenda kulala mwako, basi soma Aayaah al-Kursiy. Utaendelea kuhifadhiwa na Allaah na hutokaribiwa na shaytwaan mpaka kupambazuke. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema:
“Amesema kweli ijapo ni mwongo. Huyo alikuwa ni shaytwaan.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy.
MAELEZO
Hadiyth hii inafahamisha kuwa ni jambo limewekwa katika Shari´ah kusoma Aayah al-Kursiy wakati wa kulala na kwamba ni miongoni mwa sababu za Allaah (´Azza wa Jall) kumuhifadhi mja kutokana na shaytwaan.
Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Utaendelea kuhifadhiwa na Allaah… “
Haya ni maneno ya shaytwaan. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akayakubali na kusema:
“Amesema kweli ijapo ni mwongo. Huyo alikuwa ni shaytwaan.”
Hukumu inachukuliwa baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumsadikisha.
[1] al-Bukhaariy (3275).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 66-67
Imechapishwa: 20/10/2025
https://firqatunnajia.com/02-aayah-al-kursiy-wakati-wa-kulala/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
