Maana ya swawm kwa mujibu wa lugha ni kule kujizuia. Husemwa kuwa jua limefunga pale linaposimama. Ambaye ananyamaza huambiwa kuwa amefunga pale anapojizuilia kuongea. Amesema (Ta´ala) kuhusu Maryam (Radhiya Allaahu ´anhaa):
إِنِّي نَذَرْتُ لِلرَّحْمَـٰنِ صَوْمًا فَلَنْ أُكَلِّمَ الْيَوْمَ إِنسِيًّا
“Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwingi wa rehema ya kujizuia [na kusema], hivyo basi leo sitomsemesha mtu yeyote.”[1]
Bi maana tumefunga kwa sababu tumejizuilia kuongea. Farasi aliyegoma kutembea huambiwa kuwa amefunga.
Imekuja katika ”al-Qaamuus”:
”Swawm ni kule kujizuilia na chakula, kunywa, kuzungumza, tendo la ndoa na kutembea.”[2]
al-Fayuumiy amesema:
”Kumesemwa kuwa swawm kwa mujibu wa lugha ni kule kujizuilia kwa moja kwa moja… ”
Abu ´Ubaydah amesema:
”Kila mwenye kujizuilia na chakula, kuzungumza na kutembea basi amefunga.”[3]
al-Khaliyl amesema:
”Swawm ni kusimama bila kutenda.”
Swawm kwa mujibu wa Shari´ah ni kujizuilia kwa manuizi kutokana na vitu kutoka kwa mtu maalum na kwa sharti maalum[4].
[1] 19:26
[2] al-Qaamuus (01/1131). Tazama pia ”al-Maghrib” (247) ya al-Matwriziy.
[3] Tazama ”al-Iswbaah al-Muniyr” (352).
[4] Tazama ”al-Maghniy” (03/104) ya Ibn Qudaamah na ”ar-Rawdhwa al-Murbiy´ Sharh Zaad-ul-Mustaqniy” (01/225).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ilmaam bishay´ min Ahkaam-is-Swiyaam, uk. 07-08
- Imechapishwa: 23/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)