1 – Kumcha Allaah. Nakuusia kumcha Allaah (Jalla wa ´Alaa) katika siri na dhahiri. Huo ndio wasia wa Allaah kwa wale watu wa mwanzo na waliokuja baadaye. Amesema (Ta´ala):
وَلَقَدْ وَصَّيْنَا الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ وَإِيَّاكُمْ أَنِ اتَّقُوا اللَّـهَ
”Hakika Tumewausia wale waliopewa Kitabu kabla yenu na nanyi [pia tunakuusieni] kwamba: “Mcheni Allaah.”[1]
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ حَقَّ تُقَاتِهِ
“Enyi walioamini! Mcheni Allaah ukweli wa kumcha.”[2]
وَمَن يَتَّقِ اللَّـهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا
“Na yeyote yuleanayemcha Allaah, atamjaalia njia [ya kutoka katika matatizo].”[3]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Mcheni Allaah popote unapokuwa.”[4]
Kumcha Allaah ndio wasia wa Allaah (Jalla wa ´Alaa) kwa waja Wake na ndio wasia wa Mtume wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa ummah wake. Kwa hivyo, ee dada wa Kiislamu, ni mwenye kufanyia kazi wasia huo? Namuomba Allaah (´Azza wa Jall) anifanye mimi, wewe na waislamu wote kuwa katika wachaji Allaah.
[1] 04:131
[2] 03:102
[3] 65:02-03
[4] Ahmad, at-Tirmidhiy na wengineo. Ni nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy. Tazama ”Swahiyh-ul-Jaamiy´ as-Swaghiyr” (01/81) nr 97.
- Muhusika: Dr. ´Abdul-´Aziyz bin Daawuud al-Faaiz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tawjiyhaat wa Tanbiyhaat lil-Fataati al-Muslimah, uk. 09-10
- Imechapishwa: 27/01/2026
1 – Kumcha Allaah. Nakuusia kumcha Allaah (Jalla wa ´Alaa) katika siri na dhahiri. Huo ndio wasia wa Allaah kwa wale watu wa mwanzo na waliokuja baadaye. Amesema (Ta´ala):
وَلَقَدْ وَصَّيْنَا الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ وَإِيَّاكُمْ أَنِ اتَّقُوا اللَّـهَ
”Hakika Tumewausia wale waliopewa Kitabu kabla yenu na nanyi [pia tunakuusieni] kwamba: “Mcheni Allaah.”[1]
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ حَقَّ تُقَاتِهِ
“Enyi walioamini! Mcheni Allaah ukweli wa kumcha.”[2]
وَمَن يَتَّقِ اللَّـهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا
“Na yeyote yuleanayemcha Allaah, atamjaalia njia [ya kutoka katika matatizo].”[3]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Mcheni Allaah popote unapokuwa.”[4]
Kumcha Allaah ndio wasia wa Allaah (Jalla wa ´Alaa) kwa waja Wake na ndio wasia wa Mtume wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa ummah wake. Kwa hivyo, ee dada wa Kiislamu, ni mwenye kufanyia kazi wasia huo? Namuomba Allaah (´Azza wa Jall) anifanye mimi, wewe na waislamu wote kuwa katika wachaji Allaah.
[1] 04:131
[2] 03:102
[3] 65:02-03
[4] Ahmad, at-Tirmidhiy na wengineo. Ni nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy. Tazama ”Swahiyh-ul-Jaamiy´ as-Swaghiyr” (01/81) nr 97.
Muhusika: Dr. ´Abdul-´Aziyz bin Daawuud al-Faaiz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tawjiyhaat wa Tanbiyhaat lil-Fataati al-Muslimah, uk. 09-10
Imechapishwa: 27/01/2026
https://firqatunnajia.com/01-kumcha-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket