Tambua – Allaah akuwafikishe – ya kwamba hatua za maisha ni tano:
Ya kwanza: Kuanzia mtu anapozaliwa mpaka anapobaleghe ambako kunapitika pindi mtu anapofikisha miaka kumi na tano.
Ya pili: Kuanzia mtu anapobaleghe mpaka mwisho wa ujana wake, ambako kunapitika pindi mtu anapofikisha miaka thelathini na tano. Hii ndio miaka ya ujana.
Ya tatu: Kuanzia wakati huo mpaka pale mtu anapofikisha miaka khamsini. Kipindi hicho huitwa Kuhuulah.
Ya nne: Kuanzia miaka khamsini mpaka mtu anapofikisha miaka sabini. Hicho kipindi huitwa Shaykhuukhah.
Ya tano: Kuanzia miaka sabini mpaka mwisho wa uhai. Hiki ni kipindi kinachoitwa Haram.
Miaka tuliyoitaja inaweza kutofautiana. Ndio maana tumeigawa katika milango mitano.
- Muhusika: Imaam ´Abdur-Rahmaan bin al-Jawziy al-Hanbaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyh-un-Naa’im al-Ghamr ´alaa Mawswim-il-´Umr, uk. 45-46
- Imechapishwa: 14/02/2017
Tambua – Allaah akuwafikishe – ya kwamba hatua za maisha ni tano:
Ya kwanza: Kuanzia mtu anapozaliwa mpaka anapobaleghe ambako kunapitika pindi mtu anapofikisha miaka kumi na tano.
Ya pili: Kuanzia mtu anapobaleghe mpaka mwisho wa ujana wake, ambako kunapitika pindi mtu anapofikisha miaka thelathini na tano. Hii ndio miaka ya ujana.
Ya tatu: Kuanzia wakati huo mpaka pale mtu anapofikisha miaka khamsini. Kipindi hicho huitwa Kuhuulah.
Ya nne: Kuanzia miaka khamsini mpaka mtu anapofikisha miaka sabini. Hicho kipindi huitwa Shaykhuukhah.
Ya tano: Kuanzia miaka sabini mpaka mwisho wa uhai. Hiki ni kipindi kinachoitwa Haram.
Miaka tuliyoitaja inaweza kutofautiana. Ndio maana tumeigawa katika milango mitano.
Muhusika: Imaam ´Abdur-Rahmaan bin al-Jawziy al-Hanbaliy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyh-un-Naa’im al-Ghamr ´alaa Mawswim-il-´Umr, uk. 45-46
Imechapishwa: 14/02/2017
https://firqatunnajia.com/01-hatua-za-maisha/