736- Abu Sa´iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule atakayesoma Suurah “al-Kahf” siku ya ijumaa, basi Allaah atamwangazia nuru kati ya ijumaa mbili.”[1]
Ameipokea an-Nasaa´iy[2] na al-Bayhaqiy kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na pia al-Haakim kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kutoka kwa Swahabah. Amesema:
“Cheni ya wapokezi ni Swahiyh.”
ad-Daarimiy ameipokea katika “al-Musnad” yake kupitia kwa Abu Sa´iyd ambaye amesema:
“Yule atakayesoma Suurah “al-Kahf” usiku wa kuamkia ijumaa, basi Allaah atamwangazia nuru kati yake na kati ya Nyumba ya kale.”
Katika cheni za wapokezi wote, isipokuwa tu al-Haakim, yuko Abu Haashim Yahyaa bin Diynaar ar-Rumaaniy. Wengi wanaona kuwa ni mwaminifu. Cheni zengine zote za wapokezi ni aminifu.
[1] Swahiyh.
[2] Maneno ya mtunzi wa kitabu yanaweza kufahamika kwamba an-Nasaa´iy hakuipokea isipokuwa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) peke yake. Lakini ameipokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kutoka kwa Swahabah, kama alivofanya al-Haakim.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/455)
- Imechapishwa: 08/05/2020
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket