01. Hadiyth “Watu sampuli saba Allaah atawaweka kwenye kivuli Chake… “

326 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

سَبعةٌ يظلّهم الله في ظلِّه، يومَ لا ظِلَّ إلا ظلُّه : الإمامُ العادلُ، وشابٌّ نشأَ في عبادةِ الله عز وجل، ورجلٌ قلبه معلّقٌ بالمساجد، ورجلان تحابّا في الله؛ اجتمعا على ذلك، وتفرّقا عليه، ورجلٌ دَعَتْه امرَأة ذات مَنْصبٍ وجمالٍ؛ فقال: إنّي أخاف الله، ورجل تصدّق بصدقةٍ فأخفاها، حتى لا تعلم شمالُه ما تُنفق يمينه، ورجلٌ ذكر الله خالياً، ففاضتْ عيناه

“Watu sampuli saba Allaah atawaweka kwenye kivuli Chake siku ambayo hakuna kivuli isipokuwa Chake; kiongozi mwadilifu, kijana ambaye amekulia katika kumwabudu Allaah, mtu ambaye moyo wake umefungamana na misikiti, wanaume wawili wamependana kwa ajili ya Allaah ambapo wamekusanyika kwa ajili Yake na wakaachana kwa ajili Yake, mwanaume ambaye ameitwa na mwanamke aliye na nafasi na mzuri ambapo akasema “Mimi namuogopa Allaah, Mola wa walimwengu”, mtu ambaye ametoa swadaqah akaificha hadi mkono wake wa kushoto usijue kilichotolewa na mkono wake wa kushoto na mtu ambaye amemkumbuka Allaah akiwa peke yake macho yake yakabubujika machozi.”[1]

Ameipokea al-Bukhaariy, Muslim na wengineo.

[1] Swahiyh.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/250)
  • Imechapishwa: 03/12/2023
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy