Kuoga kumeshatajwa katika mlango wa kabla yake kupitia Hadiyth ya Salmaan al-Faarisiy, Aws bin Aws na ´Abdullaah bin ´Amr.
704- ´Abdullaah bin Abiy Qataadah amesema:
“Baba yangu aliingia wakati nilipokuwa nikioga kwa ajili ya ijumaa. Akasema: “Unaoga kwa sababu ya janaba au kwa sababu ya ijumaa?” Nikasema: “Ni kwa ajili ya janaba.” Ndipo akasema: “Basi oga mara nyingine. Kwani hakika mimi nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema: “Atakayeoga siku ya ijumaa basi atakuwa katika hali ya twahara mpaka ijumaa nyingine.” [1]
Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Awsatw”. Mlolongo wa wapokezi wake unakaribia kuwa mzuri. Ibn Khuzaymah ameipokea katika “as-Swa”iyh” yake na akasema:
“Hadiyth hii ni geni. Hakuna mwengine mbali na Haaruun (Ibn Muslim) aliyeipokea.”
Ameipokea vilevile al-Haakim kwa tamko la at-Twabaraaniy na akasema:
“Ni Swahiyh kwa mujibu wa masharti ya al-Bukhaariy na Muslim.”
Ameipokea Ibn Hibaan kwa tamko lisemalo:
“Atakayeoga siku ya ijumaa basi hatoacha kuwa na twahara mpaka ijumaa nyingine.”
[1] Nzuri.
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/441)
- Imechapishwa: 17/01/2018
Kuoga kumeshatajwa katika mlango wa kabla yake kupitia Hadiyth ya Salmaan al-Faarisiy, Aws bin Aws na ´Abdullaah bin ´Amr.
704- ´Abdullaah bin Abiy Qataadah amesema:
“Baba yangu aliingia wakati nilipokuwa nikioga kwa ajili ya ijumaa. Akasema: “Unaoga kwa sababu ya janaba au kwa sababu ya ijumaa?” Nikasema: “Ni kwa ajili ya janaba.” Ndipo akasema: “Basi oga mara nyingine. Kwani hakika mimi nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema: “Atakayeoga siku ya ijumaa basi atakuwa katika hali ya twahara mpaka ijumaa nyingine.” [1]
Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Awsatw”. Mlolongo wa wapokezi wake unakaribia kuwa mzuri. Ibn Khuzaymah ameipokea katika “as-Swa”iyh” yake na akasema:
“Hadiyth hii ni geni. Hakuna mwengine mbali na Haaruun (Ibn Muslim) aliyeipokea.”
Ameipokea vilevile al-Haakim kwa tamko la at-Twabaraaniy na akasema:
“Ni Swahiyh kwa mujibu wa masharti ya al-Bukhaariy na Muslim.”
Ameipokea Ibn Hibaan kwa tamko lisemalo:
“Atakayeoga siku ya ijumaa basi hatoacha kuwa na twahara mpaka ijumaa nyingine.”
[1] Nzuri.
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/441)
Imechapishwa: 17/01/2018
https://firqatunnajia.com/01-hadiyth-atakayeoga-siku-ya-ijumaa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)