Swali: Mwanamke kupenda sana kheri kunaweza kumpelekea akafanya baadhi ya vitu vinavyozuia ada ya mwezi ili aweze kufanya ´Umrah, kufunga au kuswali Ramadhaan. Ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Asivitumie kwa minajili ya kuswali Ramadhaan au kufunga Ramadhaan. Kwa sababu jambo lina wasaa na himdi zote anastahiki Allaah. Hiki ni kitu ambacho Allaah amewaandikia wasichana wa Aadam. Hivo ndivyo alivosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Nimefikiwa na khabari kutoka kwa madaktari waaminifu na wakweli kwamba vidonge hivi vina madhara makubwa.
Kuhusu kufanya ´Umrah huenda akaruhusiwa. Kwa sababu katika kufanya ´Umrah kuna tatizo; itampita iwapo hedhi itamjia wakati wa Ihraam kabla ya kufanya Twawaaf na akarudi nyuma kabla ya kutufu. Hapa kuna tatizo. ´Umrah huenda akaruhusiwa. Ama kwa ajili ya kufunga, kuswali na kusoma Qur-aan hapana.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa´ ash-Shahriy (71) http://binothaimeen.net/content/1636
- Imechapishwa: 28/03/2020
Swali: Mwanamke kupenda sana kheri kunaweza kumpelekea akafanya baadhi ya vitu vinavyozuia ada ya mwezi ili aweze kufanya ´Umrah, kufunga au kuswali Ramadhaan. Ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Asivitumie kwa minajili ya kuswali Ramadhaan au kufunga Ramadhaan. Kwa sababu jambo lina wasaa na himdi zote anastahiki Allaah. Hiki ni kitu ambacho Allaah amewaandikia wasichana wa Aadam. Hivo ndivyo alivosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Nimefikiwa na khabari kutoka kwa madaktari waaminifu na wakweli kwamba vidonge hivi vina madhara makubwa.
Kuhusu kufanya ´Umrah huenda akaruhusiwa. Kwa sababu katika kufanya ´Umrah kuna tatizo; itampita iwapo hedhi itamjia wakati wa Ihraam kabla ya kufanya Twawaaf na akarudi nyuma kabla ya kutufu. Hapa kuna tatizo. ´Umrah huenda akaruhusiwa. Ama kwa ajili ya kufunga, kuswali na kusoma Qur-aan hapana.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa´ ash-Shahriy (71) http://binothaimeen.net/content/1636
Imechapishwa: 28/03/2020
https://firqatunnajia.com/upambanuzi-juu-ya-kutumia-vidonge-vinavyozuia-ada-ya-mwanamke/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)