“Ndio maana ni bora kuishi katika miji ya kikafiri”

Swali: Tunaona watawala wa Kiislamu wanawadhulumu watu, wakati tunaona tofauti kabisa kwa viongozi wasiokuwa waislamu, nako ni kwamba wanataamiliana na wananchi wao kwa uadilifu na kuwapa haki zao. Kwa sababu hii baadhi ya watu wamesema kuwa ni bora kwa waislamu kuishi kwenye miji ya kikafiri. Unasemaje juu ya hilo?

Jibu: Inahitajia kuwa na uvumilifu kwa viongozi madhalimu. Muislamu kuacha nchi yake na kwenda nchi isiyokuwa ya Kiislamu kwa sababu ya dhuluma katika nchi yake, ina maana kuwa dini yake itakuja kudhurika, hata kama ataepuka dhuluma. Ikiwa kuhamia kwake katika nchi isiyokuwa ya Kiislamu hakunufaishi Uislamu wala waislamu, ni bora kwake kubaki katika nchi yake ya Kiislamu na kusubiri.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbaad
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kanda ”al-Hamalaat al-I´laaniyyah dhiwdd Hukkaam wa ´Ulamaa’ Bilaad-il-Haramayn”
  • Imechapishwa: 05/09/2020